Wednesday, October 21, 2020

SERIKALI YABORESHA KOROSHO MKOANI SINGIDA

 Singida

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele(NARI) kwa kushilikiana na Bodi ya Korosho Nchini pamoja na Serikali  ya Mkoa wa Singida imeendesha mafunzo maalum ya kilimo bora cha zao la Korosho ili kufufua zao hilo ambalo limeonyesha kusitawi kwa kiwango kikubwa katika  Mkoa huo kutokana na hali ya kijografia ya eneo hilo.

Akiongea  kwa  niaba ya  ujumbe  maalum  wa  Taasisi hizo, ofisini kwa Mkuu wa MKoa wa Singida  Dkt. Rehema Nchimbi, Afisa Mfawidhi wa Bodi ya Korosho Kanda ya Kati Bw.Ray Mtangi amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni  kuwawezesha wakulima kuingia sokoni wakiwa na Korosho zenye  uboro unaokubalika  katika masoko ya  kimataifa ili kupata bei nzuri.

Amesema mafunzo hayo yanatolewa katika wilaya zote za Mkoa wa Singida ambapo kwa sasa yameanzia Wilayani  Manyoni na yanasambazwa  katika wilaya  zote  kwa kuwa utafiti umebaini kuwa  eneo kubwa la mkoa huu linafaa kwenye kilimo cha zao la Korosho.

“Serikali imeona  ni muhimu kuelekeza nguvu zake  katika Mkoa huu  kwa kuwa  kilimo cha zao la Korosho kitakuwa  ni mkombozi wa kweli kwa wananchi wa Singida” alisisitiza Mtangi 

Pia Dkt.Geradina Mzena ambaye ni Mratibu wa zao Korosho nchini amewapongeza wadau mbalimbali ambao wameonyesha mwitikio mkubwa kutoka sehemu mbalimbali nchini kuhudhuria mafunzo  hayo ambapo amesema Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa mafunzo hayo  yatatolewa  katika kanda  mbalimnali hapa nchini ili kuleta mageuzi makubwa  katika sekta  ya kilimo kwa ujumla

Aidha ameipongeza Serikali ya Mkoa wa Singida kwa  kuwa na mkakati kabambe  wa kuanzisha  mfumo wa  mashamba makubwa ya pamoja ya bega kwa bega ambayo yameifanya Singida  kuwa  miongoni mwa  mikoa ambayo ni wazalishaji wakuu wa zao hilo

Mkuu wa Mkoa wa Singida  Dkt.Rehema Nchimbi amefafanua kuwa  hadi sasa kuna takribani ekeli 26,000 za zao la korosho ambazo zimelimwa katika Wilaya ya Manyoni, Ikungi na Itigi ambapo amesema kwa sasa serikali imesitisha ugawaji wa  mashamba ya  pamoja  kwenye wilaya ya Manyoni kwa  vile  tayari eneo kubwa  limetolewa

“Napenda kufafanua kwamba  kwa sasa   tumesitisha  ugawaji wa mashamba ya Manyoni  kwa vile eneo lote la mkoa wetu linafaa kwa kilimo hicho hivyo wananchi wanaopenda  kulima watapatiwa maeeneo hayo sehemu nyingine na kwamba  mashamba hayo ni maalum kwa ajili ya zao hilo pekee” aliongeza Dkt. Nchimbi 

Pia amesema Mkoa wa Singida ulikuwa ukisifika kwa sifa ya ukame lakini jitihada zilizofanywa na  Serikali ya Awamu ya Tano  kupitia tafiti mbalimbali zilifanya utafiti wa zao la kudumu katika Mkoa huu  kwa kuwa kulikuwa na viashilia vya mikorosho mizee hivyo ndio vilikuwa viashilia vya kugundua kuwa Korosho inastawi Singida.

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao kutoka Wizara ya Kilimo Nyaswebwa Chimagu amesema Wizara itaendelea kutoa Sera ambazo zitatasaidia  kuleta mapinduzi ya  sekta ya kilimo ili kuhakikisha kiliomo kinachangia kwenye uchumi wa Taifa na kwamba  wananchi wajitokeze kwa wingi kwenye zoezi la uelimishaji linaloendelea.

"Wito wetu kama Serikali na Wizara kwa ujumla watu waje wajifunze katika maeneo haya juu ya kilimo cha korosho" alisisitiza  Chimagu

No comments:

Post a Comment