Wednesday, October 21, 2020

RC SINGIDA -WAZEE NI BARAKA TUWATHAMINI

Manyoni

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi ametembelea Kituo cha Wazee kwenye Kijiji cha Sukamahela  Wilayani Manyoni, Mkoani Singida    na kuwapatia  mahitaji ya vyakula yenye thamani ya takribani shilingi milioni mbili ikiwa ni zawadi ya Mkoa kwa ajili ya maadhimisho ya mwaka huu ambayo hufanyika  Oktoba Mosi kila mwaka. 

Akizungumza na Wazee waishio katika Kituo hicho, amesema mageuzi  na mapinduzi ya kiuchumi yaliofanywa na Selikari ya Awamu ya Tano ni  makubwa ambayo yanalenga  kuwanufaisha wananchi wake katika umri wa sasa hadi wanapokuwa wazee.

Ameyataja baadhi ya  maendeleo hayo kuwa ni pamoja na ujenzi wa Reli ya Mwendokasi, Ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere  la kufua Umeme, utoaji wa elimu  bure kwa  wanafunzi, Ujenzi wa Vituo vya Afya na ununuzi wa ndege.

"Ndugu zangu tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu na kumshukuru baba yetu Magufuli  kwa kuwa haya yote ni kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi yetu na kunufaisha kila mtu pamoja na Wazee wa sasa  na wajao. "Alisema Mkuu wa Mkoa.

Pia, aliwaomba Watumishi wa Mungu kuwaombea Wazee ambapo alisisitiza kuwa  Wazee ni baraka na kwamba tunajifunza mambo mengi  kutoka kwao.

"Familia zenye Wazee zina baraka na mimi nataka Mkoa wa Singida uwe na historia ya kuwa na Mzee mwenye miaka mingi kuliko wote duniani" aliongeza Dkt.Nchimbi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wazee wasiojiweza Ndugu, Andrea Yohana alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa zawadi ya mbuzi, nyama ya Ng'ombe Michele, Sukari pamoja na sabuni ya kufulia ya unga.

"Tunawashukuru kwa zawadi hii mliyotupatia Mungu awabariki na kuwaongezea mlipotoa na siku nyingine mtukumbuke zaidi" aliongeza

No comments:

Post a Comment