Mkuu wa
mkoani Singida Halima Dendego, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na
Usalama ametoa kauli hiyo (27/Juni/2024)
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Stendi ya Itigi kwa
ajili kusikiliza na kero zinazowakabili wananchi wa Halmashauri ya Itigi na
kuzitafutia majawabu.
Rc Dendego
amesisitiza kuwa hatakubali Viongozi Wakuu wa Serikali watukanwe na
kudhalilishwa mkoani humo wakati yeye yupo hivyo ameonya kuwa watakaothubutu
kufanya hivyo watakiona cha moto.
Amesema kuwa
wananchi wa mkoa wa Singida ni watu wa amani na wanataka maendeleo ikiwemo
barabara maji shule afya mbolea na sio mambo ya matusi hivyo kwa yeyote anayetaka
kuvunja amani na utulivu kwa maslahi yake binafsi watashughulika nae.
“Vijana wa mkoa wa
Singida achene kukaa kimya Viongozi wanapotukwana bali muwajibu kikamilifu kupitia
mitandao ya kijamii kuhusu kazi kubwa inayofanywa na Serikali katika kuwaletea
wananchi maendeleo, Ameeleza Dendego.
Amewataka
wananchi wa mkoa wa Singida kwa umoja wao kuwakataa baadhi ya wanasiasa
wanaotaka kuwagawa wananchi kwa udini, ukabila au rangi kwa sababu Watanzania
wote ni wammoja tangu enzi na wanashirikiana katika masuala mbalimbali ya
kijamii.
Rc Dendego pia ameeleza kuwa Vyama vya siasa vilianzishwa nchini ili vishindane kwa hoja na sio matusi kwenye majukwaa na kusema ukiona baadhi ya vyama vinafanya hivyo basi havina sera na hakuna sababu ya wananchi wa mkoa huo kwenda kwenye mikutano yao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Singida Martha Malata, amewataka wananchi wa mkoa wa Singida kuwapuuza baadhi ya wanasiasa wanakuja mkoani humo kufanya siasa za uhasama na uchochezi.
Mlata amewahimiza wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya Sita kwa sababu imeonyesha dhamira ya dhati katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu katika sekta zote ikiwemo afya, elimu, maji na miundombinu.
No comments:
Post a Comment