Tuesday, December 03, 2019

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, OMARY MGUMBA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA KILIMO MKOANI SINGIDA.

 Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Singida DC mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali ya Kilimo Mazao, kilimo cha umwagiliaji na mfumo wa masoko wa mazao ya wakulima kupitia ushirika, mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akikagua bonde la Ntambuko lililopo kijiji cha Kinyeto wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akizungumza na wakulima (hawapo pichani) wanaotekeleza kilimo cha umwagiliaji kwenye bonde la Kinyeto Ntambuko Singida vijijini.

 Muonekano wa bwawa la Msange lililopo Singida vijijini. 

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini Elia Digha (kushoto) akimuonesha Naibu Waziri mradi wa skimu ya umwagiliaji unaotekelezwa kwa tija kubwa ya wakulima wa kata ya Msange mkoani Singida. 
 Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akikagua shamba la vitunguu vinavyolimwa kupitia teknolojia ya umwagiliaji kwa njia ya matone katika kijiji cha Msange mkoani Singida.

 Mkurugenzi wa kiwanda cha kukamua alizeti cha Simai, Juma Mene (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Mtinko Singida DC.

 Mbunge wa jimbo la Singida Kaskazini Justine Monko akizungumza na wananchi wa AMCOS ya Ughandi wanaojishughulisha na kilimo cha pamba muda mfupi kabla ya kumkaribisha Naibu waziri wa Kilimo.

 Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akizungumza na wananchi wa AMCOS ya Ughandi wanaojishughulisha na kilimo cha pamba halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini wakati wa ziara yake.


 Meneja wa Uhusiano na Utumishi wa kiwanda cha Mount Meru Singida Bw. Nelson Mwakabuta akisoma taarifa fupi ya kiwanda hicho mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba muda mfupi baada ya kutembelea kiwanda hicho wakati wa ziara yake mkoani Singida.

 Mkurugenzi wa kiwanda cha Singida Fresh Oil Mill, maarufu Kilimo Kwanza, Khalid Ally  Omary akimuonesha Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba (katikati) aina ya mbegu mbalimbali za alizeti zinazofaa kwa uzalishaji bora wa mafuta ya kupikia. Kushoto ni Mbunge wa jimbo la Singida Kaskazini, aliyemwakilisha mbunge wa Singida Mjini Mussa Sima.


Mkutano ukiendelea

 Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akiangalia sehemu ya uzalishaji unaofanywa na kiwacha cha kukamua alizeti cha Singida Fresh Oil Mill, maarufu Kilimo Kwanza wakati wa ziara yake.

Mkurugenzi wa kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti cha Choice Kindai, Bi. Amina Dang’ati akimuonesha Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba sehemu ya uzalishaji unaofanywa na kiwanda hicho, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya Mheshimiwa Mgumba mkoani Singida.

 Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba (watatu kutoka kushoto waliosimama) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi na uongozi wa kiwanda hicho. (kushoto waliosimama ni Mbunge wa Singida Kaskazini Justine Monko).

Kwa habari zaidi tembelea: http://www.singida.go.tz

No comments:

Post a Comment