Monday, June 04, 2018

TIMU YA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA YA MKOA WA SINGIDA (RWST) YATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA BWAWA LA SKIMU YA UMWAGILIAJI, ITAGATA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA ITIGI

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Itigi, Mhe. Pius Luhende (mwenye tai) akiongoza timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida pamoja na timu ya wilaya wakati wa kutembelea mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Itigi, Mhe. Pius Luhende (wapili kutoka kulia) akielezea maendeleo ya mradi mbele ya timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida pamoja na timu ya wilaya wakati wa kutembelea  mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

Sehemu ya Bwawa la Skimu ya Umwagiliaji, Itagata

 Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida pamoja na timu ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi wakishuka kutoka kwenye chanzo cha maji (bwawa) kuelekea kwenye mashine inayotumika kusambaza maji kupitia kwenye mifereji ya usambazaji maji yenye ukubwa wa kutosha kupeleka kwenye Mashamba.



Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida pamoja na timu ya wilaya wakitoka kukagua Mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.


AIDHA kupitia ziara hiyo, Timu ya Mkoa iliweza kukutana kikao cha pamoja na wafanyakazi wa Halmashauri ya wilaya ya Itigi wanaounda Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ili kuzungumzia maendeleo ya miradi mbalimbali ya Maji na Usafi wa Mazingira pamoja na changamoto za miradi iliyopo katika Halmashauri hiyo.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uratibu na Mipango Bw. Barthelome Temba ambaye ndiye Makamo Mwenyekiti wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida akifungua kikao cha pamoja na timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi mara baada ya kutembelea Mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Maji Mhandisi. Lydia Joseph ambaye ndiye Katibu wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja na timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi mara baada ya kutembelea Mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo kijijini ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.


Mjumbe akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja

Kikao kikiendelea

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Itigi, Mhe. Pius Luhende (wakwanza kushoto) ambaye ndiye Mwenyekiti wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja na Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Mkoa wa Singida mara baada ya kutembelea Mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo kijijini ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Singida Bw. Patrick Kasango mjumbe wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja na timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi mara baada ya kutembelea Mradi wa Skimu ya umwagiliaji uliyopo kijijini ITAGATA, katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi, wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

Wajumbe wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi wakifurahia jambo wakati wa kikao cha pamoja na timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Mkoa wa Singida.

Mjumbe wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja na timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Mkoa wa Singida.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uratibu na Mipango Bw. Barthelome Temba ambaye ndiye Makamo Mwenyekiti wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida akifunga kikao cha pamoja na timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.


Wajumbe wa Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya pamoja na Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya wilaya ya Itigi wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.

Mradi wa Ujenzi wa Bwala la Skimu ya Umwagiliaji katika Kijiji Cha Itagata Halmashauri ya wilaya ya Itigi wiliya ya Manyoni mkoani Singida una uwezo wa kuhudumia Hekta zipatazo 160 katika eneo tambarare kwa ajili ya Kilimo cha Umwagiliaji hususani zao la Mpunga, mazao ya bustani na vitalu vya kuoteshea miche ya Tumbaku kwani eneo hilo lina udongo rafiki kwa Kilimo hicho.

Imetolewa na Kitengo cha Technolojia ya Habari na Mawasiliano;
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida.

No comments:

Post a Comment