Thursday, June 07, 2018

SHINDANO LA TAHAJIA (SPELLING BEE) LAZINDULIWA RASMI MKOANI SINGIDA


Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia  uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.

Zaidi ya wanafunzi 400 wa shule za msingi na sekondari kutoka mkoa wa Singida wamependekezwa kujifunza jinsi ya kutekeleza ubora katika tahajia ya maneno kwa njia rahisi na ya ubunifu kufuatia uzinduzi wa shindano la 2018 Spelling BEE uliyofanyika leo (Juni 7, 2018) mkoani Singida.  Shindano hili litafanyika tarehe 29 Septemba mwaka huu katika chuo cha uhasibu Singida.

Akizungumza na waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo Meneja wa Shindano Bi. Upendo Mushi kutoka Cece & Daniel Enterprise amesema, Madhumuni ya mashindano haya ni kuhamasisha ubora wa mafunzo kwa njia ya ushindani wa tahajia (spelling)  katika lugha ya Kiingereza na Kiswahili, na washiriki ni wanafunzi wa darasa la nne hadi kidato cha nne kutoka shule za umma zaidi ya 32 kutoka mkoa wa Singida na inatarajiwa kuwa zaidi ya shule 15 binafsi na za kimataifa watahudhuria shindano hili.

Mkoa wa Singida  kwa ujumla una shule za msingi 551 (za umma 530 na binafsi 22) 164 (za umma 142 na 22 za binafsi) za sekondari ikiwa ni pamoja na shule 4  za wanfunzi wenye mahitaji maluum. Kitaifa shule za halmashauri za wilaya ya Itigi na Manyoni zinafanya vizuri katika mkoa wa Singida katika mitihani ya darasa la 7 na kidato cha nne. Ufaulu wa halmashauri ya  Itigi kwa mtihani ya darasa la 7 mwaka wa 2017 ilikuwa nafasi ya 56 kati ya halmshauri 186 nchini, na ufaulu wa halmashauri ya Manyoni  katika mitihani ya kidato cha nne ni nafasi 47 kati ya halmashauri 186.


Pamoja na ufaulu huu mzuri uliojionyesha kwa halmashauri hizi mbili, kiwango cha ufaulu wa shule zote za sekondari kimepanda ila katika shule za msingi za mkoa ufaulu ulishuka kwa ujumla na Mkuu wa Mkoa Dkt.  Rehema Nchimbi ameahidi kushirilkiana na wadau wote na jamii katika kuboresha elimu mkoani Singinda.  Hii ni kutokana na ujio wa  mpango wa kuboresha ubora wa elimu Tanzania – EQUIPT ambao umeanza kutekelezwa rasmi mkoani Singida kuanzia Januari 2018.

Shindano la 2018 Spelling BEE ni la kwanza kushirikisha watoto wenye mahitaji maluum Afrika Mashariki  na ambalo litajumuisha shindano la tahajia la  Kingereza na Kiswahili kwa wanafunzi viziwi.

Akizungumza katika uzinduzi wa shindano, Meneja wa shindano hili, Upendo Wanguvu alisema, "Leo tumeanza safari ya kuchochea ubora wa elimu kwa shindano la tahajia ambalo tumelenga shule za msingi na sekondari nchini Tanzania. Tunauhakika ya kwamba mashindano yetu yatahamisha ustadi wa wanafunzi kujifudisha maneno, maana ya maneno, jinsi ya kutumia maneno katika sentensi na tahaji ya maneno na hii ni mojawapo ya msingi bora wa elimu. 

"Safari yetu mwaka huu imeanza mkoani  Singida na tunatarajia ya kwamba shindano hili litajumuisha mikoa yote 31 ndani ya miaka mitatu ijayo. Aidha, uzinduzi wetu leo unafungua rasmi wigo wa kujisajili kwa shule binafsi na za kimataif kwa kutumia tovuti yetu ya www.spellingbee.co.tz ya shindano letu ” Wanguvu alisema. 

Shindano la Special Needs BEE ni la wanafunzi viziwi ambalo litafanyika kwa lugha ya Kiswahili na kingereza na wanafunzi watafanya tahajia kwa lugha ya ishara. Matuamani ya shindano hili ni kuwa zaidi wa wanafunzi 100 kutoka shule za maitaji maalum mbalimbali Tanzania watahudhuria.

Akizungumza juu ya Shindano la Special Needs BEE Bw. Yasin Mawe, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania la Viziwi alisema "Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Tanzania na Afrika Mashariki kuwa na shindano la tahajia ambalo limehusisha wanafunzi viziwi. Ushirikiano kati ya  wanafunzi wenye mahitaji maalum na wanafunzi wengine ni nguzo kuu ya maendeleo na tunafurahia ya kuwa mashindano ya 2018 Spelling BEE imejumuisha swala hili  na itajenga msingi mzuri wa ushirikiano kati ya watu wa mahitajii maalum na wengine. 

Shindano hili limeandaliwa na Cece & Daniel Enterprise wakishirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Taasisi ya Elimu ya Tanzania (TIE), Taasisi ya Africa For Inclusive Communities (AFIC), Shirika la viziwi Tanzania pamoja na ofisi ya rais TAMISEMI na ni mpango wa kipekee wa ushirikiano kati ya mashirika binafsi na mashirika ya umma (Public Private Partnership - PPP).

"Lengo kuu la PPP hii ni kuchochea tabia ya kusoma vitabu miongoni mwa wanafunzi
na tunaamini kuwa ubora wa kujifunza unapatikana pale mwanafunzi anapokuwa anajua maneno, maana yake na jinsi ya kutumia maneno haya katika sentensi. Kwa kawaida maneno yanapatikana katika vitabu na kuhamasisha wanafunzi kujifunza maneno mapya na tahajia ya maneno itasababisha kujenga tabia ya kusoma kati ya wanafunzi "alisema Bi. Upendo. 

Wito kwa wananchi wa mkoa wa Singida, wanafunzi, makampuni, wadau na wataalamu wa elimu nchini Tanzania kuunga mkono mpango huu wa kipekee wa 2018 Spelling BEE  kwa kushirikiana nao katika shindano hili.

Awali, kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana amesema kuwa, Faida ya shindano hili kwa wanafunzi ni kujifunza maneno mapya na maana zake, ambayo ni msingi bora wa elimu, Kuongeza ujasiri kwa wanafunzi kwa kusimama mbele za umma na kujieleza, Kuwajengea wanafunzi ujuzi mbalimbali katika matumizi ya lugha ni njia pekee ya kuwapata waandishi fasaha wa lugha.

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia  uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana akionyesha kitabu chenye Mwongozo wa Shindano la Tahajia waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.


Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana akionyesha kitabu chenye Mwongozo wa Shindano la Tahajia (spelling) katika lugha ya Kiingereza waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.


Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana akisikiliza maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.

Meneja wa Shindano (Event Manager-The Spelling BEE) Upendo Mushi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.

Meneja wa Shindano (Event Manager-The Spelling BEE) Upendo Mushi akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Singida Mwl. Ayoub Mchana akinakili jambo wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.


Meneja wa Shindano (Event Manager-The Spelling BEE) Upendo Mushi akionyesha kitabu chenye Mwongozo wa Shindano la Tahajia katika lugha ya Kiswahili mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.

 Meneja wa Shindano (Event Manager-The Spelling BEE) Upendo Mushi akionyesha kitabu chenye Mwongozo wa Shindano la Tahajia (spelling) katika lugha ya Kiingereza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa shindano la Tahajia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Madini Kanda ya Kati uliyopo jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.


Waandishi wa habari wakiuliza maswali

Meneja wa Shindano (Event Manager-The Spelling BEE) Upendo Mushi akijibu maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani).

Waandishi wa habari wakiuliza maswali 




Imetolewa na:
Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
SINGIDA.

No comments:

Post a Comment