Monday, April 23, 2018

DKT. REHEMA NCHIMBI AKABIDHI HATI MILIKI ZA KIMILA KATIKA KIJIJI CHA MIPILO, MKOANI SINGIDA

MKUU WA MKOA SINGIDA, DKT. REHEMA NCHIMBI AKABIDHI HATI MILIKI ZA KIMILA 21, KATIKA KIJIJI CHA MIPILO, KATA YA MAGHOJOA,  HALMASHAURI YA WILAYA YA SINGIDA, MKOANI SINGIDA 20/04/2018



Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiwakabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilaya ya Singida, mkoani Singida. 










Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akimkabidhi Hundi mwananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilaya ya Singida, mkoani Singida.  



Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhe. Elias Tarimo (watatu kutoka kushoto) akimkabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila Mchungaji wa Kanisa na wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilaya ya Singida, mkoani Singida.  







Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Monko Justine Joseph akimkabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila kwa mwananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilaya ya Singida, mkoani Singida.  





Mheshimiwa Diwani akimkabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila mwananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilaya ya Singida, mkoani Singida. 


Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiwasisitizia jambo wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida juu ya faida na Umuhimu wa kupima Mashamba yao na kupata Hati za Hakimilizi za Kimila.









Wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa sherehe za kukabidhi Hati za Kimila Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida.



Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Singida Mjini Elias Tarimo akizungumza jambo wakati wa sherehe za kukabidhi Hati za Kimila kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida.



Wananchi wakimsikiliza kwa makini Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Singida Mjini Elias Tarimo wakati akizungumza jambo katika sherehe za kukabidhi Hati za Kimila kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida.



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Rashid M. Mandoa akifuatilia jambo wakati wa zoezi la ugawaji wa Hati za Kimila kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida. 


Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Monko Justine Joseph akizungumza na wananchi wa kata ya Maghojoa na kuagiza maeneo yote ya wanakijiji hao yasiyo na mgogoro kupimwa kwa gharama za Mbunge. Mhe. Monko aliahidi.

MAPOKEZI


Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akisalimiana na kamati ya mapokezi mara baada ya kuwasili eneo la tukio kwaajili ya kuwakabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida.




Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akibebeshwa Dhawa ishara ya makaribisho mema ya sherehe ya kukabidhi Hati ya Hakimiliki ya Kimila kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida. 



 Wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida wakishangilia jambo wakati wa hafla ya Hati ya Hakimiliki ya Kimila.


Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (wakatikai) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakulima waliopatiwa Hati za Kimila wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida 

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumalizi kwa zoezi la ugawaji wa Hati miliki za Kimili kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Singida Mjini Mhe. Elias Tarimo pamoja na Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Monko Justine Joseph wakifurahia jambo wakati Dkt. Nchimbi akizungumza na waandishi wa Habari 

AWALI ALIPOKUWA NJIANI


Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (mwenyekilemba cheupe) akizungumza na wananchi kwa lengo la kuwaelewesha nia madhubuti ya zoezi hilo la ugawaji Hati za Kimila kwa wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida. 



Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akisalimiana na wananchi wa Kata ya Maghojoa katika Halmashauri ya wilayani ya Singida, mkoani Singida mara baada ya maongezi mafupi yenye kuwajengea uelewa wa umuhimu wa Hati ya Hakimiliki ya Kimila.

MPANGO WA USIMAMIZI WA MATUMIZI BORA YA ARDHI
Ardhi ni Rasilimali ya msingi na jukwaa la maisha ya binadamu inayotumiwa kwa kuzalisha mazao, kufugia mifugo, kuhifadhia wanyamapori na misitu, kujenga nyumba na huduma mbalimbali. Ili kukidhi mahitaji haya hapana budi watumiaji wa ardhi kuweka utaratibu wa mipango ya matumizi ya ardhi.

Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Na. 6 ya Mwaka 2017 imeweka misingi na malengo ya kupanga matumizi ya ardhi kuwa ni:-
A. Kuwezesha ufanisi na usimamizi muafaka wa matumizi ya ardhi
B. Kuwezesha wamiliki na watumiaji wa ardhi kuwa na matumizi na uzalishaji bora wa mazao
C. Kuwezesha matumizi endelevu ya ardhi
D. Kuwezesha na kuasisi mfumo wa kuzuia migogoro ya matumizi ya ardhi
E. Kuweka mfumo wa kuratibu ujumuishi wa kisekta katika ngazi mbalimbali ikiwemo miundo ya           Kisiasa na kiutawala
F. Kuweka mfumo wa kuhusisha misingi ya maendeleo ya Taifa iliyoainishwa katika sera za Serikali 

Faida za Hati za Hakimiliki za Kimila:-
i. Kuongeza thamani ya Ardhi inayomilikiwa
ii. Kupunguza migogoro ya Ardhi baina ya wakulima na wakulima, wafugaji na wakulima, vijiji na vijiji
iii. Kutumia Hati za Hakimiliki za kimila kama dhamana
iv. Kutumia Hati za Hakimiliki za kimila kwa kupata mikopo katika Taasisi mbalimbali za Kifedha (Mabenki, Saccos, VICOBA n.k)
Kuwawezesha wakulima kuitunza Ardhi vizuri na kuongeza uzalishaji wa mazao
vi. Kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi kisheria

No comments:

Post a Comment