Tuesday, July 04, 2017

HABARI PICHA; NAMNA SINGIDA ILIVYOHITIMSHA KWA UFANISI NA KUKABIDHI MWENGE WA UHURU SIMIYU.



Mkuu wa Mkoa wa Simgoda Dkt Rehema Nchimbi akijiandaa kuukabidhi mwenge wa uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka, katikati yao ni Mkimbiza Mwenge Kitaifa Bahati Lugodisha akiwa na mwenge wa uhuru.




Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhandisi Jakson Masaka akiukabidhi mwenge wa uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi mara baada ya kuhitimisha mbio za mwenge wa uhuru kwa halmashauri saba za Mkoa wa Singida, ili aweze kuukabidhi mkoa wa Simiyu.



Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiupokea mwenge wa uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama kabla ya kuendelea na itifaki ya kuukabidhi kwa mkoa wa Simiyu.


Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina Mageni Lutambi akiwa na mwenge wa uhuru kabla ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi kuendelea na itifaki ya kuukabidhi kwa mkoa wa Simiyu.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akisoma taarifa ya mbio za mwenge wa uhuru Mkoani Singida kwa Mwaka 2017 kabla hajaukabidhi kwa Mkoa wa Simiyu, kushoto kwake ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Amour Hamad Amour.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiagana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Amour Hamad Amour kabla ya kukabidhiwa Mkoani Simiyu.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Amour Hamad Amour ‘akinyakua’ pamoja na askari wa Mkoa wa Singida kama ishara ya kuagana kwa upendo kabla ya kukabidhiwa Mkoani Simiyu.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Amour Hamad Amour akiwa na wakimbiza mwenge kitaifa kwa pamoja ‘wakinyakua’ pamoja na askari wa Mkoa wa Singida kama ishara ya kuagana kwa upendo kabla ya kukabidhiwa Mkoani Simiyu.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Debora Mgiligimba akiongoza askari wengine kuwaaga wakimbiza mwenge kitaifa waliofanya kazi nzuri mkoani Singida katika halmashauri saba.


Mkuu wa Mkoa wa Simgoda Dkt Rehema Nchimbi akijiandaa kuukabidhi mwenge wa uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka, katikati yao ni Mkimbiza Mwenge Kitaifa Bahati Lugodisha akiwa na mwenge wa uhuru.

No comments:

Post a Comment