Thursday, May 04, 2017

WANANCHI WATOE USHIRIKIANO UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA.



Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akisikiliza kwa maelezo ya tathmini ya athari za mazingira na kijamii kwa mradi wa bomba la mafuta, wa kwanza kulia kwake ni Katibu Tawala Mkoa Dkt Angelina Lutambi. 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi (katikati) akisikiliza kwa maelezo ya tathmini ya athari za mazingira na kijamii kwa mradi wa bomba la mafuta, wa kwanza kulia kwake ni Katibu Tawala Mkoa Dkt Angelina Lutambi na kushoto ni Mtathmini wa mazingira Bi Saada Juma kutoka kampuni ya JSB. 
Wananchi wa Wilaya tatu za Makalama, Iramba na Singida Mkoani Singida ambazo bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga linapita wanapaswa kutoka ushirikiano wa kutosha katika hatua zote za ujenzi wa bomba hilo ili wanufaike na fursa zitakazopatikana kwa uwepo wa mradi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo katika kikao cha tathmini ya athari za mazingira na za kijamii katika mradi wa bomba la mafuta ambapo watathmini watapita maeneo yote ambapo bomba hilo litapita ili kupata maoni yao ili yaweze kuzingatiwa wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

Dkt. Nchimbi amesema wananchi wanapaswa kuwajulisha watathmini hao kila kitu kuhusu hali ya mazingira na kijamii ili mradi huo usiharibu mazingira au upunguze baadhi ya athari wakati wakujenga bomba hilo.

Ameongeza kuwa wananchi wasiwe na wasiwasi kuhusu fidia kwa maeneo ambapo bomba litapita kwakuwa watalipwa vizuri fidia zao na hivyo wanapaswa kuruhusu mradi huo upite katika maeneo yao bila wasiwasi na pia wasianze kuendeleza maeneo ambayo wamesikia mradi utapita kwa kigezo tu cha kupata fidia kubwa.

Kwa upande wake Mtathmini wa Mazingira Saada Juma kutoka kampuni ya JSB ambayo inafanya tahmini hiyo amesema wanatekeleza matakwa ya kisheria katika kufanya tahmini hiyo na wataifanya kwa kasi kubwa ili ujenzi rasmi wa mradi uwahi kufanyika.

Saada amesema mradi huo utakua kambi mbalimbali na kwa mkoa wa Singida kambi itakuwa katika kata ya Msisi ambapo uwepo wa kambi hiyo utaongeza uchumi wa kata na wilaya hiyo.

Amesema vijana wa Singida wajiandae kwa ajili ya kupata ajira mbalimali katika mradi huo, baadhi ya miundombinu itaboreshwa pamoja na uchumi kukukua kwa kuuza bidhaa na kutoa huduma kwa watakaokuwa wakiishi katika kambi hiyo.

Tathmini ya athari za mazingira na za kijamii kwa wilaya za Singida, Mkalama na Iramba ambapo mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda mpaka  Tanga itaana mapema wiki ijayo.
Ramani inayoonyesha maeneo ya wilaya tatuza Mkoa wa Singida ambapo tathmini ya athari za mazingira na kijamii kwa mradi wa bomba la mafuta litakalopita kutoka Uganda hadi Tanga. 

Mtaalamu Bw. Lalit Kumar kutoka kampuni ya RSK  itakayohusika na ujenzi wa bomba la mafuta litakalopita kutoka Uganda hadi Tanga. 

Wadau wa sekta mbalimbali zinazohusika na mazingira kutoka mkoa wa Singida wakifuatilia kwa umakini maelezo ya tathmini ya athari za mazingira na jamii kwa ujenzi wa bomba la mafuta litakalopita kutoka Uganda hadi Tanga.

No comments:

Post a Comment