Thursday, September 22, 2016

MWENGE WATEMBELEA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI NANE WILAYANI SINGIDA.



Miradi ya maendeleo 15 yenye thamani ya shilingi bilioni 8,391,131,054 imetembelewa na mwenge wa uhuru katika halmashauri za manispaa na singida wilayani Singida.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo amesema miradi hiyo imejikita katika sekta za afya, maji, elimu, barabara, kilimo, ufugaji, miradi ya akina mama na vijana pamoja na vilabu vya wapinga rushwa na madawa ya kulevya.

Tarimo amesema katika halmashauri ya manispaa miradi iliyowekewa mawe ya msingi ni pamoja na stendi mpya ya mabasi yaendayo mikoani ambapo mradi huo una thamani ya shilingi bilioni 3,726,072,678 na mradi wa barabara ya kiwango cha lami wenye thamani ya bilioni 2,694,339,096.

Aidha katika upande wa kuwajengea uwezo vijana kiuchumi manispaa imeendelea kutenga asilimia kumi ya bajeti ya mwaka ili kuwawezesha vijana mafunzo ya namna ya kubuni miradi na kuiendeleza.

Katika mapambano dhidi ya Ukimwi Tarimo amesema manispaa imeweza kuanzisha vituo kumi vya kupima Ukimwi na kutoa ushauri nasaha, vituo 26 vya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa motto na vine vya kutoa dawa za kufubaza VVU.

Amesema kwa kipindi cha Januari 2015 mpaka septemba 2016 wakazi wa manispaa 19,591 wamepima VVU ambapo waliopatikana na maambukizi ya VVU ni 1,124.

Kwa upande wa ugonjwa wa maralia ambapo kauli mbiu yake ni “wekeza katika maisha ya baadaye tokomeza maralia” manispaa imefanikiwa kupunguza maambukizi na vifo vitokanavyo na ugonjwa huo kutoka asilimia kumi mwaka 2014 hadi asilimia 3.7 mwaka 2015 kutokana na juhudi za manispaa za kutoa elimu ya kuteketeza mazalia ya mbu na matumizi ya vyandarua vilivyowekewa da ya viuatilifu.

Tarimo amefafanua kuwa wananchi wanaelimishwa na kushauriwa kuwahi hospitali pindi wanapoona dalili za homa na si kujinywea dawa bila maelekezo ya wataalamukwani si kila homa ni malaria na endapo watagundulika kuwa na ugonjwa wa malaria wanashauriwa kutumia dawa mseto na kukamilisha dozi.

Kwa upande wa halmashauri ya singida, mwenge wa uhuru umezindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi minane yenye thamani ya milioni 989,039,279 ambapo nguvu ya wananchi ni shilingi milioni 84,186,600, halmashauri ya wilaya ni milioni 21,607,450,  wahisani ni  76,742,000 na serikali kuu 806,503,229  pamoja na kuhamasisha wananchi juu ya umoja, mshikamano na uzalendo.

Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa maji wa kijiji cha Itaja wenye thamani ya shilingi milioni 411,405,887 uliokamilika mwezi Mei pamoja na miundombinu ya nyumba ya mashine, ufungaji wa jenereta na pamu za kusukumia maji, ujenzi wa njia kuu ya kupeleka maji kwenye matanki na ujenzi wa mtandao wa kusambaza maji kwenye vituo vya kuchotea maji.

Mradi huo utakaonufaisha wakazi wa Itaja kwa kuwapatia maji safi na salama umekabidhiwa kwa jumuiya ya watumia maji iliyopewa mafunzo ya uendeshaji na iko chini ya uangalizi kwa kipindi cha miezi sita.

Naye Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru George Jackson Mbijima ameweka jiwe la msingi ujenzi wa kiwanda cha kusindika mbogamboga kijiji cha msange na kuwashauri wanakikundi kuendeleza usindikaji wa mazao hayo kwani ni changamoto kwa wakulima kutokana na kuharibika haraka.

Amesema mradi ukisimamiwa utakuwa mkombozi wa wakulima kutokana na kuwa wakulima wengi hulalamika kuharibika mazao kutokana na kukosa masoko haraka hasa kwa mazoa ya mbogamboga, aidha mradi utatengeneza ajira kwa vijana na akina mama wengi wa kijiji cha msange na halmashauri ya Singida.
 
Ameongeza kwa kusisitiza kuwa mradi utaboresha afya ya wanajamii wanaouzunguka na kuwashukuru wahisani waliotoa shilingi milioni 47,000,000, huku halmashauri ikichangia milioni 2,000,000 na wananchi milioni 4,046,000 katika kufanikisha ujenzi wa kiwanda hicho.

Miradi mingine iliyotembelewa na mwenge wa uhuru halmashauri ya Singida ni pamoja na klabu ya wapinga rushwa shule ya sekondari Mughamo, mradi wa vijana wa ufugaji nyuki na uhifadhi wa mazingira kijiji cha Msikii, Mradi wa utunzaji wa mazingira sekondari ya Mrama, ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Mwahango na ujenzi wa ghala la kuhifadhia alizeti Kata

No comments:

Post a Comment