Baraza la wafanyakazi la Sekretarieti ya Mkoa wa Singida limefanyika leo asubuhi katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida.
Moja ya ajenda zilizopewa kipaumbele na wajumbe wengi ni mpango wa Mafunzo kwa wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekretarieti ya Mkoa wa Singida wakifuatilia ajenda za baraza hilo.
Wajumbe hao wamesisitiza umuhimu wa mafunzo kwa wafanyakazi kwani unaongeza ujuzi na ufanisi wa utendaji kazi wa wafanyakazi.
No comments:
Post a Comment