Mahakimu na Wasimamizi wa Sheria Mkoani Singida wametakiwa kuepuka vitendo vya kupokea rushwa ambayo unaosababishwa upindishwaji wa Sheria ili kuwatendea haki wananchi huku wakihimizwa kusaidia kutatua migogoro kwa njia ya usuluhishi.
Maelezo hayo yametolea leo na Jaji Mstaafu Fatuma Massengi
wakati wa kilele cha wiki wa Sheria inayoadhimishwa kila tarehe 1 Februari
Nchini, maadhimisho ambayo Mkoa wa Singida zimeadhimishwa katika viwanja vya
Mahakama ya Mkoa iliyopo mjini Singida.
Jaji Massengi amesema katika vitabu vya dini vimeeleza
kwamba Mahakimu watakuwa wa mwisho kuingia mbinguni kwa kuwa maswali yatakuwa
mengi hasa kwa wale ambao hawakuwatendea haki wanaanchi.
Aidha amewaasa Mahakimu kutenda haki na kusimamia Sheria kwa
kuwa kazi hiyo ni kazi ya Mungu na ni msingi wa Maendeleo ya nchi ambapo kama
Sheria itapindishwa itasababisha kudumaza uchumi wa nchi.
"Tuache kupokea rushwa kwa kuwa inadidimiza uchumi,
napenda kuwakumbusha Mahakimu kuhakikisha wanatenda kazi ya Mungu bila upendeleo,
vitabu vya dini vinaeleza kwamba Mahakimu watakuwa wa mwisho kuingia mbinguni
kwa kuwa watakuwa na maswali mengi ya kujibu" Alisema Jaji Fatuma.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewaomba
wanasheria wa Serikali na Binafsi kuambatana naye kila wiki ya tatu ya kila
mwezi kwenda Wilayani kutatua kero za Wananchi badala ya kusubiri maofisini.
Aidha amewataka Maafisa wa Mahakama kuongeza jitihada ya
kutoa elimu kwa wananchi ambao hawajui umuhimu wa kutatua migogoro yao nje ya
Mahakama ili kuwapunguzia gharama kupeleka mashtaka Mahakamani ambayo yangeweza
kutafutiwa kwa usuluhishi.
"Tumeanzisha utaratibu wa kuwafuata wananchi walipo
kwenda kusikiza changamoto zinazowakabili hivyo niwaombe mawakili wa Serikali
na Binafsi tuwe tunaambatana kwenda kutatua migogoro kwa njia ya usuluhishi
walipo wananchi". Serukamba
Hata hivyo amepongeza Mahakama kwa kuwa mabingwa wa kutumia
teknolojia ya Habari kutatua kuendesha mashtaka na kupunguza mrundikano wa kesi
katika Mahakama zao.
Naye Hakimu mkazi wa Mahakama kuu ya Singida Allu Nzowa
amesema Mahakama imejipanga kuhakisha kwamba katika mwaka mpya wa Sheria
watahakikisha haki za watu zinapatikana kwa wakati.
Nzowa amewataka wananchi kuepuka migogoro kwa sababu imekuwa
chanzo cha kudidimiza uchumi kwa wananchi na kuleta umaskini kwakuwa watu
wanashindwa kuendelea kuzalisha au kufanya biashara kwa sababu ya migogoro.
Awali Mkuu wa Mashtaka Mkoa wa Singida Juma Hasani Salige alieleza kwamba wananchi
wanapata changamoto kuendesha migogoro kwa gharama kubwa huku ikisababisha
kupungua na kudhoofika kwa uchumi wao, huku mwakilishi wa Chama cha Mawakili wa
kujitegemea (LLS) Salma Musa, aliomba
wanasheria binafsi washirikishwe kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia ya
usuluhishi na kupatiwa jengo la ofisi Mkoani hapa.
MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA
No comments:
Post a Comment