Watumishi wa umma wametakiwa kuandaa bajeti zitakazogusa wanufaika wa jinsi zote kwa usawa, hususan makundi maalumu wakiwemo wazee, wanawake na watu wenye ulemavu, ili kuhakikisha maendeleo jumuishi katika jamii.
Wito huo umetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro , Dkt. Mussa Ali Mussa, wakati akiwa mgeni rasmi katika kikao kazi cha maandalizi ya bajeti yenye mrengo wa kijinsia kilichowakutanisha Maofisa Maendeleo ya Jamii, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya, Mipango na Uratibu, Sehemu ya Biashara na Uwekezaji pamoja na Maafisa Habari wa Mikoa.
Kikao hicho kinafanyika mkoani Morogoro kwa siku mbili kuanzia tarehe 2 hadi 3, 2026, kikilenga kuwajengea washiriki uwezo wa kuandaa na kutekeleza bajeti zinazozingatia mahitaji ya makundi yote katika jamii.
Dkt Mussa amesema ni muhimu katika uandaaji wa bajeti hizo kushirikiana na makundi maalumu ambayo ni mahsusi kwa ajili ya bajeti hiyo ili kupata mawazo na vipaumbele kutoka kwao ikiwemo mahitaji yao kwa wakati husika sambamba na miradi wanayoipa kipaumbele na ambayo wanaweza kuifanyia kazi kwa muda mfupi na kuwapa mafanikio.
Kadhalika amewataka viongozi hao kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha wanawaunga mkono wanufaika wote wa Mikopo ya asilimia kumi kwa kununua bidhaa zao ikiwemo mchanga,kokoto mawe katika matumizi ya ujenzi wa majengo ya serikali na mengineyo kwa lengo la kuwaongezea kipato,ari ya kufanya kazi kwa bidii sambamba na kuwawezesha kurejesha mikopo yao kwa wakati unaotakiwa na kuweza kukopa kwa awamu nyingine.
Bi.Lilian Liundi, mwezeshaji wa mafunzo ya bajeti yenye mrengo wa jinsia kutoka NIRAS, aliwasilisha mada mbalimbali kwa wajumbe wa kikao hicho ikiwemo mafunzo ya uelewa wa jinsi na jinsia,mahitaji ya msingi na ya kimkakati ya jinsia,kadhalika jinsi ya kutengeneza bajeti yenye mrengo wa kijinsia katika jamii yenye tamaduni imara zinazokinzana na sera za usawa wa kijinsia.
Kadhalika aliwasilisha mada ya nyenzo zinazopaswa kutumika katika uandaaji wa bajeti yenye mrengo wa kijinsia ikiwemo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dira ya Taifa 2050,Sheria ya fedha,Sheria ya Ununuzi,na nyinginezo.
Kwa ujumla, mafunzo hayo yanatarajiwa kuleta matokeo chanya kwa kuongeza usawa na ujumuishi katika utoaji wa huduma za umma, kuboresha upangaji wa vipaumbele kulingana na mahitaji halisi ya makundi maalumu, kuimarisha utekelezaji wa sera na sheria za kitaifa, kuongeza kipato kwa wanufaika wa mikopo ya asilimia kumi, kuimarisha uwajibikaji na ushirikiano wa wadau wa maendeleo, kubadili mitazamo hasi ya kijamii kuhusu masuala ya kijinsia, pamoja na kuongeza tija na mafanikio ya miradi ya maendeleo katika jamii.



Dkt. Mashinji ameongeza kuwa Wilaya imefanya juhudi kubwa katika kushughulikia suala hilo, hatua iliyosababisha kumualika Mkuu wa Mkoa kuja kusaidia kusuluhisha changamoto hiyo kwa kiwango cha juu zaidi, akisisitiza kuwa kila mwananchi atapata haki yake kwa mujibu wa sheria na taratibu.
Kwa mujibu wa taarifa za Wilaya ya Manyoni, mgogoro wa ardhi katika maeneo ya miradi ya umma umedumu kwa muda mrefu kutokana na kukosekana kwa uhakiki wa kina wa umiliki wa ardhi kabla ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hali iliyosababisha sintofahamu kati ya wananchi na Serikali, na hivyo kuilazimu Serikali ya Mkoa kuingilia kati ili kuhakikisha haki za wananchi zinalindwa sambamba na utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya maendeleo.











