Tuesday, January 31, 2023

RAS SINGIDA ATAKA MRADI WA SHULE BORA UTENGENEZE MFUMO WA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU

KATIBU Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko, ameuagiza Mradi wa Shule Bora unaotekelezwa katika mikoa tisa (9) nchini kutengeneza mfumo wa kutoa mafunzo kwa walimu wa Mkoa wa Singida ili kuinua viwango vya elimu mkoani hapa.

Akifungua mkutano wa uhamasishaji wa Programu ya Shule Bora kwa wasimamizi na wahariri wa vyombo vya habari leo, amesema walimu watakaopewa mafunzo hayo nao watakwenda kuwafundisha wenzao.

"Kila Halmashauri kuwe na 'trainers' ambapo kutatafutwa 'centre'  walimu watakuwa wanakutana na hivyo wataguswa walimu wengi kwa wakati mmoja na mpango huu uanze mara moja mwezi Februari mwaka huu," amesema.

Mradi wa Shule Bora umelenga kuiunga mkono Serikali ya Tanzania katika kuinua kiwango cha elimu jumuishi pamoja na kuweka mazingira salama ya kujifunzia kwa wanafunzi wa kike na kiume katika shule za Serikali zilizopo katika mikoa ya  Singida, Dodoma, Simiyu, Tanga, Mara, Rukwa, Katavi, Pwani na mkoa wa Kigoma.


Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoani Singida Samweli Daniel, akitoa taarifa ya Mradi wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni.

Afisa Elimu Mkoa wa Singida Maria Lyimo, akizungumza wakati wa mkutano huo.


Meneja Mawasiliano wa Shule Bora Bw. Raymond Kanyambo, akizungumza wakati wa Mkutano huo.

Mwandishi wa Habari Seif Takaza akizungumza wakati wa mkutano huo.




No comments:

Post a Comment