Hali ya Chama cha Walimu cha akiba na mikopo cha Wilaya ya
Iramba (CHAMWAI) imeendelea kuwa tete
baada shauri lao na Mkuu wa Mkoa wa Singida kuahirishwa ili kutafutwe nyaraka
husika.
Shauri hilo limesogezwa mbele mpaka tarehe 31 Januari
2023 ili kutoa fursa kwa wahusika kuandaa
nyaraka ambapo ameelekeza kuletewa
jalada la chama hicho lililopo CRDB likiwa na nyaraka zote muhimu,
Wakurugenzi wa Halmashauri ya Iramba na Mkalama kuleta nyaraka zote zenye
uhusiano na chama hicho.
Kauli hiyo imetolewa leo na RC Serukamba alipokutana na Walimu
wastaafu katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo ambapo walieleza kwamba madai
yao ni zaidi ya Milioni 300.
RC Serukamba alieleza kwamba analazimika kuahirisha kikao
hicho ili kutoa nafasi ya kuzipata nyaraka zote tokea chama hicho
kilipoanzishwa lengo likiwa sio kupata madeni ya walimu hao bali kuangalia
fedha nyingine za chama hicho ambazo zimeibwa.
Amesema ni kweli yapo madeni yanayotakiwa kulipwa na
Halmashauri ya Iramba zaidi ya Milioni 20 na Mkalama zaidi ya milioni 14 lakini
inawezekana zipo fedha nyingine ambazo CRDB wanatakiwa kutoa maelezo jinsi
walivyozitoa pasipo kufuata utaratibu.
"Mikopo yote ina utaratibu wake hivyo nataka kuona muhutasari
unaoruhusu kuchukuliwa mkopo huo na masharti kama yamefuatwa" alisema
Serukamba
"Tukisema tuwaambie Wakurugenzi waliotumia fedha za
chama hicho watafanya hivyo lakini inawezekana walimu wanapata hela zao lakini
chama kinaendelea kupoteza haki zao" Aliendelea kueleza Serukamba
Hata hivyo RC amemuagiza DC wa Iramba Seleimani Mwenda
kuhakikisha siku ya kujadili tena swala hilo wawepo waliokuwa viongozi wa
CHAMWAI wa awali ili kujibu hoja zitakazojitokeza.
Kwa upande wa msemaji wa wastaafu hao Mlogwa Temaeli amesema wameridhishwa na utaratibu uliowekwa na RC Serukamba wa namna ya kutatua swala lao huku akieleza kwamba wamepata matumaini mapya.
MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA
No comments:
Post a Comment