Serikali ya
mkoa wa Singida imewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Polisi wa Wilaya mkoani
humo kuwasaka na kuwakamata watu wote (vikundi) waliochukua mikopo ya asilimia
10 kwenye Halmashauri mkoani Singida ili warejeshe kulingana na kiasi kilichokubaliwa
katika mkataba wa mkopo.
Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego, ametoa kauli hiyo
katika kikao cha Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Iramba cha kujadili hoja za
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024.
Rc Dendego
ametoa mfano kwa Halmashauri ya Iramba pekee zaidi ya Milioni 118
hazijarejeshwa mpaka sasa na kusisitiza kuwa tatizo lazima litafutia ufumbuzi
kwa wahusika kukamatwa ili warejeshe mikopo hiyo.
“Nataka Dc na OCD
muwasake popote walipo watu waliokopeshwa fedha hizo ili wazirejeshe ili
wananchi wengine wakopeshwe,” Amesisitiza Dendego.
Aidha, RC
Dendego amesisitiza kuwa vikundi vyote vya wanufaika wa mikopo hiyo kuanza
marejesho haraka iwezekanavyo na wote watakaokaidi agizo hilo
wakamatwe na kuchukuliwa hatua kwa muujibu wa kisheria taratibu na kanuni za
mkataba.
Mkuu huyo wa
mkoa pia amewaagiza Maafisa Maendeleo ya Jamii mkoani humo washirikiane na
Viongozi wengine katika kusaka Vikundi vilivyokopeshwa fedha hizo na
kuzirejesha haraka vinginevyo nao watawajibishwa mpaka hapo vikundi hivyo
vilipe fedha hizo kwa sababu wao wanavijua.
Naye, Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Innocent Msengi, ameunga mkono hoja ya
wanachama wa vikundi vilivyokopeshwa fedha za Halmashauri kusakwa ili warejeshe
fedha hizo.
Msengi
amesema fedha hizo zinazodaiwa ni nyingi hivyo lazima nguvu ya ziada itumike
ili kuhakikisha waliokopeshwa wanazirejesha ili wananchi wengine waweze
kunufaika na mikopo hiyo ya Halmashauri.
Mwenyekiti
huyo pia amemshukuru Rais Samia kwa kuipatia Halmashauri hiyo zaidi ya shilingi
Bilioni Tatu kwa ajili ya kutelekeza miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika
sekta za afya na elimu.
Mkaguzi Mkuu Ofisi ya Mdhibiti wa Hesabu za Serikali mkoa wa Singida Othman Jumbe akizungumza kwenye kikao hicho.



No comments:
Post a Comment