Saturday, March 23, 2019

VIONGOZI NA WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KAMPENI INAYOENDELEA YA KUSAJILI WATOTO WENYE UMRI WA CHINI YA MIAKA MITANO.


Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa, Balozi Dk. Augustine Mahiga (MB), akimkabidhi mtoto wa umri chini ya miaka mitano cheti cha kuzaliwa, wakati wa uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi ulihusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.

SERIKALI imewataka viongozi na wananchi kwa ujumla kutambua kuwa mfumo thabiti wa usajili na vifo ni kichocheo cha ukuaji kwa sekta ya viwanda nchini, hivyo wana wajibu kushiriki kikamilifu kampeni inayoendelea ya kusajili watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano. 

Wito huo umetolewa (21/03/2019) na Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa, Dk. Augustine Mahiga (MB), wakati akizungumza kwenye sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano. Uzinduzi huo uliohusu mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika katika kituo cha zamani cha mabasi ya mikoani mjini Singida.

Mheshimiwa, Dk. Augustine Mahiga (MB), amesema kuwa mwekezaji akitaka kujenga kiwanda cha bidhaa za watoto mkoani Singida, ni lazima apate takwimu sahihi za watoto walipo katika mkoa huu, na pia mikoa jirani. Pengine hata akahitaji takwimu za watoto nchi nzima. 

Amesema, mwekezaji anaweza kuhitaji kujua kiwango cha ukuaji wa idadi ya watu (‘population growth rate’). Sababu kubwa ikiwa ni kupata uhakika wa soko la bidhaa zake kwa miaka ijayo. 

“Mpango tunaouzindua leo (21/03/2019), una majawabu ya mahitaji yote niliyoyataja, hivyo kuanzia leo viongozi na wananchi sote  tutambue umuhimu wa kusajili watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano” Dk. Mahiga. 

Akisisitiza, Dk. Mahiga amesema, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimabli kwa lengo la kuleta maboresho ya mfumo wa usajili kupitia mkakati wa kitaifa wa usajili  matukio muhimu ya binadamu na takwimu. 

 Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa, Balozi Dk. Augustine Mahiga (MB), akizungumza na wananchiwakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano. Uzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida. 

Kitendo hiki ni maamuzi ya Serikali ya awamu ya TANO, natuhinishe kitendo cha uandikishaji na muono wa Rais wetu Mheshimiwa Dk. John Pombe Magufuli. Uandikishaji ulikuwepo lakini umepewa umuhimu na kiongozi ambaye anamaono makubwa kuhusu watoto na maendeleo yao. Na unaposema mtoto unasema mama. Maendeleo hayaji bila takwimu”.  

“RITA ikiwa kama moja ya taasisi katika wizara yangu, tunafanya kazi kwa karibu pamoja na wadau wengine, kuhakikisha kwamba mkakati huu wa usajili unakubalika na kueleweka kwa wadau mbalimbali ili kuweza kuingizwa katika mipango ya nchi”, Dk. Mahiga. 

Aidha, Dk. Mahiga amesema ataendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo ya mpango wa usajili wa watoto huku akisisitiza kuwa utamaduni wake ni kufuatilia jambo kwa karibu na hapendi kuzindua kitu ambacho hakitafanikiwa. 

Awali, Kaimu Kabidhi Wasii Mkuu, Bi. Emmy K. Hudson, amesema huduma za usajili wa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano sasa umesongezwa  karibu zaidi kwa  wananchi. Sasa utafanyikia kwenye ofisi za watendaji wa kata na vituo vya afya vinavyotoa huduma za afya za mama na mtoto.

Kwa mujibu wa Kaimu Kabidhi Wasii  Mkuu Bi. Emmy, amesema utekelezaji wa kampeni hii katika mikoa ya Singida na Dodoma awamu ya kwanza hadi sasa zaidi ya watoto 2,987,629, wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa.

Kupitia mpango huu, wastani wa kitaifa umepandishwa kwa zaidi ya asilimia  15 awamu ya kwanza na kufikia zaidi ya asilimia 38.5. Tunategemea takwimu hizi kubadilika muda mfupi ujao baada ya kumaliza bakaa la watoto wasio na vyeti vya kuzaliwa katika mikoa ya Dodoma na Singida ambao ni zaidi ya watoto 665,060.

Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) umefanikiwa kusajili Watoto Milioni tatu na kuwapatia vyeti vya kuzaliwa bila ya malipo kupitia Mpango wa usajili wa Watoto walio na umri chini ya miaka mitano unaoendelea kutekelezwa katika Mikoa kumi na mitatu Tanzania Bara.

MUHIMU: 
(Cheti hiki kinatolewa bila malipo kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, cheti cha kuzaliwa sio uthibitisho wa Uraia).

MATUKIO KATIKA PICHA

 Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa, Dk. Augustine Mahiga (MB), akisalimiana na Mheshimiwa Meya wa Manispaa ya Singida Alhaji Mbua Chima mara baada ya kuwasili katika eneo la tukio la sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.

 SEHEMU YA MEZA KUU

 Kikundi cha Mbalamwezi kutoka Manispaa ya Singida kikiburudisha wakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.



 Mkuu wa Wilaya ya Singida Mheshimiwa Mhandisi Pascas Muragili akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.

 Kaimu, Kabidhi Wasii Mkuu, Bi. Emmy Hudson, akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.



 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju, akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.

  Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa, Balozi Dk. Augustine Mahiga (MB),  akifurahia jambo wakati Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju alipokuwa akizungumza na wananchi katika sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.




 Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Rehema Nchimbi akizungumza na wananchi wakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.


   

Shamla shamla za hapa na pale zikiendelea wakati wa sherehe za uzinduzi wa mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitanoUzinduzi huo umehusisha mkoa wa Singida na Dodoma, umefanyika mkoani Singida.

    
   


IMETOLEWA NA;
KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO
OFISI YA MKUU WA MKOA
SINGIDA

No comments:

Post a Comment