Saturday, October 13, 2018


MKUU wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, ameagiza halmashauri zote za wilaya na manispaa mkoani Singida, kuanzisha madawati  yatakayo simamia  mawasiliano  kati ya TAREA (Tanzania Renewable Energy Association) na halmashauri hizo, yatakayohusu upatikanaji na usambazaji wa nishati mbadala.

Dkt Nchimbi, ametoa  wito huo jana wakati akizindua maonesho  ya nishati mbadala ya siku mbili yaliyofanyika kwenye viwanja vya Peoples klabu mjini hapa. Alisema dawati hilo liwe kwenye ofisi za halmashauri, na lisimamiwe kikamilifu na maafisa maendeleo ya jamii ili iwe na mawasiliano endelevu na TAREA.
  
Katika hatua nyingine, ameziagiza halmashauri hizo kuhakikisha zinaweka umeme wa nishati mbadala katika shule za msingi, sekondari, mabweni na vyanzo vya maji.

“Tutumie umeme wa nishati mbadala katika shule zetu, wanafunzi waweze kutumia mwanga huo kujisomea bila matatizo. Kupitia mwanga huo, wataweza kuinua taaluma zao na hivyo kufanya vizuri zaidi kwenye mitihani yao” Dkt. Nchimbi.

Dk.Nchimbi alitumia fursa hiyo kukishukru chama cha  TAREA, kwa kuleta maonyesho hayo mkoani Singida. Amedai kupitia maonyesho hayo wananchi watapata elimu na maarifa juu ya umuhimu wa kutumia nishati mbadala kwenye shughuli mbalimbali zikiwemo za kiuchumi.

Kwa upande wake mwenyekiti  wa TAREA kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kilichopo katika manispaa ya Morogoro, Profesa Amini Kweka, alisema TAREA ni chama ambacho kimeundwa na watu mbalimbali na taasisi zisizo za kiserikali zinazovutiwa na malengo ya TAREA. 

Alitaja baadhi ya  majukumu yao ikiwa ni pamojana na  kueneza maarifa na maelezo juu ya teknolojia za nishati jadidifu, nakutoa ushauri wa kitaalamu juu ya mambo ya nishati jadidifu, na kushiriki kuandaa bidhaa zenye viwango bora.

TAREA ni Tanzania Renewable Energy Association,  ni jumuiya ya watu ambao wanavutiwa na nishati jadidifu na ambao wanatambua uzuri wa teknolojia za nishati jadidifu (nishati itokanayo na jua, upepo, na maji). TAREA ilisajiliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani na kupata nambari ya usajiri SA 10900 mnamo tarehe 17 Mei, 2001.

MATUKIO KATIKA PICHA







  



 

WASHIRIKI WAKIWA KATIKA ZIARA YA KUTEMBELEA KWENYE MITAMBO YA NISHATI JADIDIFU ITOKANAYO NA JUA PAMOJA NA MTAMBO UNAOSUKUMA MAJI KWA NJIA YA UPEPO KATIKA KIJIJI CHA PUMA NA KIMBWI HALMASHAURI YA IKUNGI MKOANI SINGIDA. 13/10/2018








Imetolewa na;
KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO
OFISI YA MKUU WA MKOA 
SINGIDA

No comments:

Post a Comment