Monday, March 19, 2018

WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI WILAYANI IRAMBA WACHANGIA MADAWATI 300 KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI


WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI WILAYANI IRAMBA WACHANGIA MADAWATI 300 KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI.



Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Wakili. Boniface Engelberth Kalikona wamekabidhiwa madati 300 yenye thamini ya shilingi za Kitanzania milioni 30 kutoka kwa wachimbaji wadogo wadogo katika Mgodi wa Sekenke Nkonkilangi Wilaya ya Iramba kwa ajili ya shule za sekondari na misingi wilayani Iramba ili kuunga mkono jitihada za serikali. 

Akizungumza juzi na wachimbaji wadogo katika machimbo ya Sekenke yaliyopo katika Kijiji cha Nkonkilanga, Kata ya Ntwike, Tarafa ya Shelui, Wilayani Iramba alipokuwa katika viwanja vya mgodi wa Sekenke Mkuu wa Wilaya ya Iramba amewashukuru sana kwa ushirikiano wao na kwa kujitoa kuchangia madawati.

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Iramba amewaomba wachimbaji wadogo wadogo kuifadhi na kutunza mazingira ili yawe mazuri kwa lengo la kuepukana na Magonjwa ya milipuko.

Makundi ya wachimbaji waliochangia madawati ni Sekenke One  Madawati 115,  Iramba Nkulu Madawati 20, Iramba Kenkang’ombe Madawati 135,  Mgodi wa Mzizini Madawati 10 na hapa kazi tu Madawati 20.

PICHA ZA MADAWATI YALIYOPOKELEWA NA MKUU WA WILAYA IRAMBA
  Madawati yaliyochangiwa na kikundi cha wachimbaji wadogo IRAMBA KENKANG'OMBE mgodi wa Sekenke jumla ya Madawati 135.

   Madawati ya kikundi cha wachimbaji wadogo SEKENKE ONE mgodi wa Sekenke jumla ya Madawati 115.

Madawati yaliyochangiwa na kikundi cha wachimbaji wadogo IRAMBA NKULU mgodi wa Sekenke jumla ya Madawati 20.
  Madawati yaliyochangiwa na kikundi cha wachimbaji wadogo HAPA KAZI TU mgodi wa Sekenke jumla ya Madawati 20.
 
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula (mwenye kofia ya njano waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wachimbaji wadogo wadogo walioungana na kuunda vikundi mbalimbali vinavyojihusisha na shughuli za uchimbaji mkoani Singida.

No comments:

Post a Comment