Tuesday, July 25, 2017

YALIYOJIRI ZIARA YA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI MKOANI SINGIDA - JULAI 25, 2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wakazi wa Itigi mara baada ya kuzungumza nao na kuzindua barabara Manyoni-Itigi-Chaya, ambapo pamoja na mambo mengine ameagiza ujenzi wa barabara ya Chaya-Nyaua yenye kilomita 85 na ujenzi uanze ndani ya siku 45 ili barabara hiyo ikamilike kwa kiwango cha lami.

#Leo tuomboleza kumbukumbu za Mashujaa, tumeamua kufanya Maadhimisho hayo kwa kusaidia shughuli za kijamii- Rais Dkt. Magufuli.

#Mkoa wa Singida ulikuwa na KM 3 tu za barabara za lami, lakini leo una KM 495 za barabara za lami - Rais Dkt. Magufululi.

#KM 495 nimezishiriki kuzijenga nikiwa Waziri wa Ujenzi - Rais Dkt. Magufuli.

#Tangu nimeanza ziara yangu Biharamuro mpaka hapa Itigi, nimezindua zaidi ya KM 707 za barabara za lami zenye thamani ya zaidi ya Bil. 860 - Rais Dkt. Magufulu.

#Fedha zote za ujenzi wa barabara hizo zimetolewa na Serikali kwa asilimia 100 -  Rais Dkt. Magufuli.

#Tumeamua kulipa malimbikizo ya  madeni ya wakandarasi  zaidi ya Tsh. Tril. 1 - Rais Dkt. Magufuli.

#Tanzania ni miongoni mwa nchi chache Afrika zilizotoa umeme 45% kwa wananchi wake - Rais Dkt. Magufuli.

#Itigi wala Manyoni hapakuwa na umeme, lakini leo wana umeme - Rais Dkt. Magufuli.

#Tunataka tuwe na umeme wa uhakika ili Tanzania ya viwanda ifanikiwe - Rais Dkt. Magufuli.

#Ndoto ya Baba wa Taifa ya kuifanya Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi lazima tuitimize kwa vitendo - Rais Dkt. Magufuli.

#Zaidi ya Watumishi 3000 wameshahamia Dodoma - Rais Dkt. Magufuli.
 
#Makao Makuu yakishakuwa Dodoma inamaana na miji ya karibu nayo itakuwa kama Makao Makuu ya Nchi - Rais Dkt. Magufuli.

#Wakati wa kukaa kwenye magenge na kusikiliza maneno kwamba mtaletewa vya bure umeshapita - Rais Dkt. Magufuli.

#Nataka niwatendee Watanzania haki na kuwaeleza kweli - Rais Dkt. Magufuli.

#Ndio maana nawaambia Watanzania kwamba Tanzania tumeibiwa vya kutosha - Rais Dkt. Magufuli.

#Nataka niijenge Tanzania mpya - Rais Dkt. Magufuli.

#Mimi ni CCM lakini nafanya kazi za Watanzani wote, sibagui - Dkt. Magufuli.

#Mwaka huu tumetangaza nafasi 50 elfu za manesi, madaktari na walimu - Rais Dkt. Magufuli.

# Ajira zilikuwa hazitangazwi kutokana na ajira kuzibwa na wafanyakazi hewa zaidi ya 19,000 - Rais Dkt. Magufuli.

#Tanzania tunajenga Reli ya aina yake Afrika nzima ambayo itatumia umeme - Rais Dkt. Magufuli.

#Nataka Tanzania iwe ya kisasa - Rais Dkt. Magufuli.

#Tukishakuwa na miundombinu ya lami,  nchi itatajirika kutokana na biashara zitakazofanyika - Rais Dkt. Magufuli.

#Tanzania ni kati nchi 5 Afrika zinazokuwa kwa kasi kiuchumi, ambapo Tanzania inakua kwa 7% - Rais Dkt. Magufuli.

#Ndugu zangu wa Itigi tuanze kulima Uwele, Mtama, Viazi na Mihogo ambavyo vinastahimili mvua kidogo - Rais Dkt. Magufuli.

#Tumefuta tozo zaidi ya 80 kwenye kilimo - Rais Dkt. Magufuli.
 
#Tumefuta zaidi ya tozo 7 kwenye mifugo na zaidi ya tozo 5 kwenye uvuvi - Rais Dkt. Magufuli.

*Imeandaliwa na Idara ya Habari - MAELEZO.*

No comments:

Post a Comment