Monday, November 14, 2016

WAGONJWA WA KISUKARI SINGIDA WAADHIMISHA SIKU YA KISUKARI DUNIANI KWA KUPIMWA MACHO .

Daktari bingwa wa macho Mkoani Singida Ngh'ungu Kuzenza akimfanyia uchnguzi wa macho mgonjwa wa kisukari katika kuadhimisha siku ya kisukari duniani. 


Baadhi ya wagonjwa wa kisukari wa kliniki ya Hospitali ya Mkoa wa Singida wakisubiria kufanyiwa uchunguzi wa  macho katika kuadhimisha siku ya kisukari duniani.





Wagonjwa wa kisukari Mkoani Singida leo wamefanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya macho na daktari bingwa wa macho katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa kisukari duniani ikiwa na kauli mbiu ya ugonjwa wa kisukari na magonjwa ya macho.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Singida Dokta Ramadhani Kabala amewaambia wagonjwa wa kisukari waliohudhuria kufanyiwa uchunguzi wa macho kuwa maadhimisho hayo mwaka huu yamelenga kuzuia wagonjwa wasiathirike zaidi na magonjwa yatokanayo kisukari.

Dokta Kabala amesema ugonjwa wa kisukari hushambulia zaidi macho, figo na moyo hivyo serikali imeweka mkazo wa kuwafanyia uchunguzi ili kubaini tatizo ili wapatiwe matibabu mapema au kuzuia yasitokee kabisa kwa kufuata kanuni na taratibu za ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa ugonjwa wa kisukari unawakumbusha watu kuishi kwa kufuata kanuni bora za afya kama kula mlo kamili, kula matunda badala ya juisi zilizotengenezwa viwandani, kufanya mazoezi na kupunguza vilevi na sigara hivyo wagonjwa wa kisukari hawana togauti na watu wengine isipokuwa wao hushauriwa kufuata kanuni hizo kwa umakini mkubwa.

Dokta Kabala amewakumbusha kutumia dawa kwa kufuata usahuri wa daktari wao pamoja na kuhudhuria kliniki za kisukari kwakuwa kliniki hizo zinawasaidia katika kushauriana namna bora ya kuishi kwa kufuata masharti wananyopewa pamoja kuelimishanzaidi juu ya ugonjwa huo.

Naye Daktari bongwa wa macho Mkoani Singida Dokta Ngh’ungu Kuzenza amesema utaratibu huo unasaidia kuzuia au kupunguza madhara ya ugonjwa wa kisukari kwakuwa wengi watatambuliwa kabla hawajafikia hatua ya kupofuka.

Dokta Kuzenza ameongeza kuwa changamoto kubwa ni watu wengi kutopima ugonjwa wa kisukari mapema mpaka wanapougua na hivyo kujikuta wameshaathirika macho ndipo hutafuta huduma.


Kwa upande wake mmoja kati ya wagonjwa wa kisukari 76 waliopata huduma ya kibingwa ya macho Bi Asha Selemani Waziri Mkazi wa Iguguno ameema serikali imeweka utaratibu mzuri wa kuwapima macho ili waweze kupata tiba mapema.

Bi Waziri ameiomba serikali kuendelea kuweka utaratibu wa kuwapima wagonjwa wa kisukari magonjwa mbalimbali kama moyo na figo huku akiwashauri wagonjwa wa kisukari kufuata ushauri wanaopewa na  wataalamu wa afya.
Daktari bingwa wa macho Mkoani Singida Ngh'ungu Kuzenza akimfanyia uchnguzi wa macho mgonjwa wa kisukari katika kuadhimisha siku ya kisukari duniani.


















Baadhi ya wagonjwa wa kisukari wa kliniki ya Hospitali ya Mkoa wa Singida wakisubiria kufanyiwa uchunguzi wa  macho katika kuadhimisha siku ya kisukari duniani.

No comments:

Post a Comment