Friday, November 04, 2016

BENKI YA CRDB YASAIDIA UJENZI WA BWENI LA WASICHANA LILILOTEKEA KWA MOTO

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Geoffrey Mwambe akipokea mifuko ya simenti 73 kutoka kwa Meneja wa Benki ya CRDB tawil la Manyoni Bwana Richard Karata.

Na Veronica-Manyoni
Benki ya CRDB tawi la Manyoni imetoa mifuko 73 ya saruji yenye thamani ya Sh. Mil 1,168,000 ili kuchangia ujenzi wa bweni la Wasichana wa kidato cha tano na sita la Mwanzi Sekondari iliyopo Wilayani Manyoni, Mkoani Singida lililoteketea kwa moto mwezi Septemba. 
Meneja tawi la CRDB Manyoni Bw. Richard Karata Mchango huo amewasilisha mchango huo jana ambapo mchango huo umetolewa na Watumishi wa Benki ya CRDB tawi la Manyoni walioguswa na tatizo la wanafunzi wa Kidato cha tano na sita wa Mwanzi Sekondari wanaoishi katika mazingira magumu kwa kukosa bweni.

Msaada huo umepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Geoffrey Idelphonce Mwambe ambaye amewashukuru sana wafanyakazi hao kwa kujitolea katika kusaidia sekta ya elimu katika ujenzi wa bweni lililoteketea kwa moto.

“Nawaomba wananchi na wadau wengine wa maendeleo waendelee kutuunga mkono katika juhudi za ujenzi wa bweni hili la wasichana wa Mwanzi Sekondari ili waepukane na adha wanayoipata sasa”, ameongeza Mhe. Mwambe. 

Bweni la Wasichana wa Shule ya Sekondari Mwanzi Wilayani Manyoni liliteketea kwa moto usiku wa tarehe 9 Septemba, 2016 na kuwaacha Wanafunzi hao wakiwa hawana mahali pa kulala. 

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Geoffrey Mwambe akipokea mifuko ya simenti 73 kutoka kwa Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Manyoni Bwana Richard Karata.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Geoffrey Mwambe akipokea mifuko ya simenti 73 kutoka kwa Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Manyoni.

No comments:

Post a Comment