Saturday, October 01, 2016

WANANCHI WAASWA KUTOA USHIRIKIANO KWA UTAFITI WA UKIMWI.



Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi  Mathew J Mtigumwe akifungua mkutano wa wadau wa utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi.

Wananchi wameaswa kutoa ushirikiano kwa wataalamu watakaofanya utafiti wa viashiria vya ukimwi utakaofanyika nchi nzima na kuhusisha kaya elfu 16 na kuwafikia watanzania elfu 42,000 wakiwemo watoto elfu nane.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha shirika la ICAP-Tanzania linalofadhili utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi Mama Mihayo M Bupamba amesema utafiti umepokelewa kwa hisia tofauti ukipotoswa kuwa utahusika kila kaya wakati sio kweli.

Mama Mihayo amesema utafiti utahusisha kaya chache tu za Tanzania nzima ambapo ambapo kaya hizo zitaombwa ridhaa na utafiti utafanyika kwa usiri na kufuata sera na taratibu za wizara ya afya, mila, desturi, usiri na utaalamu wa hali ya juu utazingatiwa hivyo wasiwe na wasiwasi.

Ameongeza kuwa lengo utafiti huo ni kuendleza utafiti wa kuoima hali ya ukimwi kila baada ya miaka mine ambapoa mara ya wisho ulifanyika mwaka 2012.

Mama Mihayo amesema utafiti huu utahusisha hali ya ukimwi, maambukizi mapya, wingi wa kinga ya mwili, wingi wa virusi vya ukimwi kwa watu wanaoishi na maambukizi ya Virus vya ukimwi, Uwezo wa mwili wa kumeng’enya dawa za kupunguza makali pamoja na magonjwa ya kaswende na homa ya ini.

Ameongeza kuwa utafiti utasaidia kupata taarifa sahihi kwakuwa nyingi zimekuwa zikipatikana kwa wale tu wanaoenda kupima hospitali hasa wajawazito au wagonjwa bila kuhusisha ambao hawajafika kupima.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew J. Mtigumwe amesema utafiti ni wa muhimu sana na kuwasihi wananchi wa Mkoa wa Singida kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wataalamu hao.

Mhandisi Mtigumwe amesema utafiti huo utasaidia watunga sera waweze kupanga kupanga mikakati mizuri zaidi ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi.

Ameongeza kuwa utafiti huo ni wa kipekee kwakuwa utahusisha rika zote tofauti na tafiti zilizotangulia pia utahusisha vipimo vingi na majibu kutolewa hapohapo.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano kutoka shirika la Icap Mama Mihayo Bupamba akitoa mada katika kikao cha wadau wa utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi.

Wadau wa utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi wakisikiliza kwa umakini kikao cha utafiti huo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi  Mathew J Mtigumwe (katikati) akifuatilia mada katika mkutano wa wadau wa utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi kushoto kwake ni katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimaliwatu Buhacha B. Kichinda na Kulia kwake ni Kaimu Meneja wa ofisi ya Takwimu Mkoa wa Singida Naing'oya Kipuyo.

No comments:

Post a Comment