Saturday, June 11, 2016

ZIARA YA MKUU WA MKOA WA SINGIDA KIJIJI CHA GUMANGA KUTEMBELEA WAKULIMA WA MBOGAMBOGA NA MATUNDA

























Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe: Mathew Mtigumwe (katikati) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Christopher Ngubiagai  (nyuma yake) na ujumbe kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi (mbele).


Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe: Mathew Mtigumwe na ujumbe wake wakimsikiliza Mkulima waliyemkuta shambani.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe: Mathew Mtigumwe(Kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Christopher Nguabiagai wakimsikiliza mmoja wa wajumbe wa kikundi cha wanawake wajasiriamali wakati akiwaelekeza namna ya kutengeneza tomato sauce na tomato paste.

Na Omary Mtamike, Mkalama

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa  Injinia Mathew Mtigumwe amesisitiza wakulima kujiunga na vikundi vidogo  na vikubwa ili waweze kupatiwa Mikopo itakayowawezesha kuendeleza miradi yao kwa urahisi.
Mtigumwe ameyasema hayo alipofanya ziara mwisho wa wiki katika Kiwanda cha kusindika zao la nyanya kinachotarajiwa kuanza kufanya kazi  muda wowote kuanzia sasa ambapo kitasaidia wakulima wanaolima zao hilo katika kata ya Gumanga na maeneo ya karibu kupata sehemu ya kuuza mazao yao.
“Kupitia kiwanda hiki sasa mtaweza kuzalisha nyanya kwa wingi kwa sababu mmeshapata sehemu ya kuuza badala ya awali ambapo mlikuwa mkiuza kwa hasara au kuyaacha yakiharibika shambani”. Alisema Mtigumwe.
Akisisitiza kuhusu suala hilo la kujiunga na vikundi Meneja wa Shirika la viwanda vidogo (SIDO) mkoani Singida , Shoma Kibende alisema shirika hilo lina uwezo wa kukopesha kila mwanachama aliyepo kwenye kikundi kiasi cha shilingi laki tano hivyo alishauri wanakijiji wa kata ya Gumanga wajiunge kwenye vikundi ili iwe rahisi kwao kukopesheka.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida alimmwagia sifa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Christopher Ngubiagai na safu yote ya watendaji wake kwa kazi nzuri ya kutekeleza maagizo yote wanayopewa huku ikiongoza katika kila kampeni za kitaifa zinazotangazwa ikiwemo ya maabara pamoja na madawati.
“ Kwa kweli Mkalama mnastahili sifa sana kwa sababu kila kampeni ya kitaifa mmekuwa mkiongoza kwa Mkoa wote wa Singida na nimeambiwa hata hili la madawati mbali na kuongoza mpaka hivi sasa, mtalimaliza rasmi tarehe 15 mwezi huu, hongereni sana”,  Alisema Mtigumwe.
Aliongeza juu ya hilo kwa kuwashauri wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri za wilaya nyingine za mkoa huo kufika katika Wilaya ya Mkalama na kujifunza  ni namna gani wanaweza kutekeleza maagizo kwa mafanikio.



Hili si ndoo ya Maji bali ni mtambo wa kutengeneza mvinyo kwa kutumia nyanya kama ulivyowasilishwa na kikundi cha Wanawake wajasiriamali katika Kata ya Gumanga.

Hili ndio jengo la Kiwanda cha Kusindika Nyanya ambalo linatarajiwa kukamilika na kuanza kazi  muda wowote kuanzia sasa.

No comments:

Post a Comment