Tuesday, June 10, 2014

MBIO ZA MWENGE WA UHURU ZAKAMILIKA MKOANI SINGIDA, MWENGE WAKABIDHIWA MKOA WA DODOMA (Makabidhiano katika picha).


























Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Singida zimekamilika leo na Kukabidhiwa Mkoa wa Dodoma, Wilaya ya Chemba katika kijiji cha Kinyamshindo.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan ameukabidhi mwenge wa uhuru kwa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Rehema Madenge.


Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan akimkabidhi mwenge wa uhuru  Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Rehema Madenge.

Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2014 Ndugu Rachel Stephen Kassanda ameushukuru Uongozi wa Mkoa wa Singida kwa ushirikiano wa kipekee waliouonyesha.

Kassanda amewataka wananchi wa Mkoa wa Singida kulinda na kuthamini miradi ya maendeleo iliyozinduliwa, kufunguliwa na kutembelewa na Mwenge.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2014 Ndugu Rachel Stephen Kassanda akimshukuru Katibu Tawala Mkoa wa  Singida kwa ushirikiano wa kipekee

Pia amewasihi wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi utakapowadia wakati wa kupiga kura ya maoni ili kupata katiba mpya ya nchi yetu.

Kassanda amesisitiza suala la amani kuwa ni msingi wa maendeleo ya taifa letu hivyo wananchi wanapaswa kuhakikisha wanaitunza amani ya nchi yetu huku wakidumisha ushirikiano na umoja.
Wakimbiza Mwenge Mkoa wa Singida, wajumbe wa kamati ya uratibu wa mbio za mwenge wa uhuru Mkoa wa Singida na Askari waliokimbiza mwenge Mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya Pamoja.


Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Singida wakishuhudia makabidhiano ya Mwenge kwa Mkoa wa Dodoma.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Rehema Madenge wakipongezana baada ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru.


Mratibu wa Mbio za Mwenge wa uhuru Mkoa wa Singida Henry Kapella (wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wakimbiza Mwenge Kitaifa.

No comments:

Post a Comment