Wednesday, November 30, 2022

Kila Mtoto kupata Chanjo ya Polio awamu ya Nne - Serukamba

 

Wananchi Mkoani Singida wametakiwa kuhakikisha wanawapatia watoto wao wenye umri wa miaka chini ya mitano chanjo ya matone dhidi ya Ugonjwa wa Polio itakayotolewa kuanzia tarehe Moja hadi Nne Desemba, 2022.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ya Mkoa (PHC) Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba amewataka wazazi na jamii kwa ujumla kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa chini ya miaka mitano anapata chanjo ili kuwa salama na watu wengine.

Aidha RC Serukamba amefafanua kwamba jumla ya watoto ambao wanatarajia kupata chanjo ni 443,230 ambapo  Iramba ina watoto 65,074  Singida Dc watoto 690,557 Manyoni 55,825 Manispaa ya Singida  45,722 Ikungi 97,575 Mkalama 58,905 na Itigi watoto 51,072.

"Tayari vifaa na chanjo vimekwisha wasili katika vituo mbalimbali vya Afya na Zahanati ambapo huduma nyingine zitakuwa zikitolewa kwa njia ya mkoba nyumba kwa nyumba mtoto baada ya mtoto" alisema Serukamba.

Hata hivyo amewataka wakuu wa Wilaya kusimamia zoezi hilo kuhakikisha chanjo hiyo inatolewa na inawafikia idadi iliyopangwa katika Wilaya.

Amesema chanjo inayotolewa imedhibitishwa kwamba ni salama hivyo Serikali haitawavuliwa watu wenye nia mbaya ya kuwapotosha wananchi.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Kamati ya Mkoa ya ulizi na usalama, viongozi wa Dini mbalimbali, Taasisi, muwakilishi kutoka Wizara ya Afya TAMISEMI na  muwakilishi kutoka Shirika la Afya duniani.

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba.


Kikao kikiendelea



No comments:

Post a Comment