Katibu Tawala huyo wa mkoa ametoa maagizo hayo (tarehe 31
Mei, 2024) wakati anafunga mashindano UMITASHUMTA yaliyofanyika katika viwanja
vya Shule ya Sekondari Mwenge kwa kushirikisha wanafunzi zaidi ya 700 kutoka
Halmashauri za Mkoa wa Singida.
Dkt. Fatuma Mganga amesema anaimani kubwa uchaguzi wa
wanafunzi watakaowakilisha mkoa kwenye mashindano hayo watarudi na makombe ya
kutosha katika kila aina ya mchezo.
Amesisitiza maandalizi kwa wanafunzi hao yawe bora ikiwemo
matumizi ya vifaa na zana za kisasa ili mkoa ushike nafasi ya kwanza kwenye
mashindano hayo.
Katibu Tawala huyo pia amewataka Maafisa michezo wa Halmashauri kutumia kauli mbiu ya mwaka huu ya UMITASHUMTA kupitia fani ya uimbaji (kwaya) kutangaza mafanikio ya utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa katika awamu ya sita ikiwemo shule (majengo ya madarasa), hospitali, miundombinu ya barabara, kilimo, maji na sekta mbalimbali zinazotekelezwa mkoani Singida.
Aidha, kwa mwaka 2023 mkoa wa Singida ulishika nafasi ya Tisa kitaifa na kutoa wanafunzi 12 waliounda Timu ya Taifa.
Naye Afisa Michezo, Utamaduni na Sanaa wa Mkoa wa Singida,
Amani Mwaipaja, amesema mashindano hayo mwaka huu yalianza kufanyika ngazi ya
shule, kata, Wilaya na sasa mkoa kwa kushindania michezo saba ambayo ni mpira
wa miguu, netboli, mpira wa mikono, mpira wa wavu, mpira wa kikapu na riadha.
Amesema kumekuwa na Halmashauri zenye wanafunzi wenye
mahitaji maalum ambao pia walishirikishwa kwenye mashindano kutoka Manispaa ya
Singida kulikuwa na timu ya mpira wa miguu kwa wanafunzi viziwi, Ikungi na
Iramba kulikuwa na wanafunzi wenye uoni hafifu na ualbino.
Mwaipaja amesema mashindano haya ambayo yaliwashirikisha
jumla ya wanafunzi 732 kutoka Halmashauri za Wilaya ya Iramba, Ikungi, Singida
DC, Mkalama, Manyoni, Itigi na Manispaa ya Singida yalianza Mei 28, 2024 na
kuhitimishwa Mei 31, mwaka huu ambapo waliweka kambi katika Shule ya Sekondari
Mwenge iliyopo Manispaa ya Singida.
Amesema baada ya mashindano haya kuliundwa timu ya mkoa
iliyowajumuisha wanafunzi 120 pamoja na walimu timu itakayoandaliwa kwa ajili
ya mashindano ya kitaifa yatakayofanyika katika Mkoa wa Tabora.
Mwaipaja akizungumza maendeleo ya michezo ya UMITASHUMTA na
UMISSETA kwa mwaka 2023, amesema Mkoa wa Singida ulipata mafanikio makubwa
ikiwamo kupata kombe la mshindi wa pili mpira wa miguu na Netball kwa
wasichana.
No comments:
Post a Comment