Sunday, June 02, 2019

MASHINDANO YA UMISSETA NGAZI YA MKOA, YAMEZINDULIWA KWA KISHINDO, MKOANI SINGIDA


Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, amezindua mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.

Akizindua mashindano hayo, Mkuu wa mkoa wa SINGIDA Dkt. REHEMA NCHIMBI amehimiza suala la nidhamu kwa wachezaji na kusisitiza kuwa  anaimani kuwa wachezaji watakaochaguliwa kwenda kuuwakilisha mkoa kwenye mashindano ya taifa yatakayofanyika mkoani Mtwara watafanya vizuri ili kuibuka na medali nyingi na kuuletea heshima mkoa wa SINGIDA. 

Dkt. Nchimbi amesema, Michuano hii ndio itakuwa chemichemi ya kuchagua  wachezaji ambao wataenda kuuwakilisha mkoa wa SINGIDA katika michuano ya Umisseta ngazi ya Taifa huko mkoani MTWARA na Viongozi wa mkoa wa SINGIDA wamesema wanaimani kubwa kuwa timu ambayo itachaguliwa itakuwa bora na itafanya vyema kwenye michuano hiyo.

"Hatuna timu nyingine, timu ni hii hapa, ninyi ndio timu yetu ya mkoa wa Singida. mimi sina timu nyingine, na sio timu ya mzaha ni timu ya ushindi"
"Mnauwezo, na lazima mkafanye vizuri, mtakapo kuwepo na sisi tupo. tunachotaka ni kimoja tuu... ushindi. " Amesema Dkt. Nchimbi

Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt.  ANGELINA LUTAMBI akizungumza wakati wa uzinduzi huo amesema, mwaka huu mkoa wa Singida umejipanga vizuri katika michuano hiyo ya UMISSETA na kuwataka wachezaji wote walioingia kambini hapo kucheza kwa bidii na nidhamu ya hali ya juu katika michuano hiyo ili kujitangaza na kuuletea sifa mkoa wa Singida katika sekta ya michezo nchini.

"Tunaamini vijana wetu watakapo kamilisha makambi yao hapa na kwenda  kule Mtwara, mwaka huu tutafanya vizuri sana. Ninaamini kwamba tutakapofanya vizuri katika mashindano haya, ndio itakuwa tiketi yetu yakuonekana zaidi kitaifa". Amesema Dkt. Lutambi

Naye, Afisa Michezo na Utamaduni wa mkoa wa Singida Bw. HENRY KAPERA amefafanua jinsi michauno hii ilivyoibua vipaji vya wachezaji wengi ambao wengine wanasakata kabubu kwenye timu kubwa hapa nchini.

"Kuna wachezaji wetu walishacheza michezo ya umiseta miaka MINNE iliyopita, siku hizi wanacheza katika vilabu vikubwa nchini akiwepo Raphael Loti aliyekuwa mchezaji kutoka Halmashauri ya Wilaya Itigi mkoani Singida ambaye kwa sasa anayechezea timu ya Yanga" Amesema Kapera

Pia amemtaja Jeremia Juma anayechezea Tanzania Prisonal ambaye naye alipitia katika michuano hiyo ya Umiseta kutoka mkoani Singida na kuwahimiza wanamichezo hao kujituma wakati wote ili vipaji vyao vipate kuonekana na hatimaye kuwa sehemu ya ajira.

Katika kuhakikisha michuano hii inafanyika kwa utulivu wa hali ya juu Mkuu wa mkoa wa SINGIDA Dkt. REHEMA NCHIMBI amechangia shilingi laki TANO kama hatua ya kuwapa hamasa wachezaji kujiandaa vyema na michuano ya mkoa na ya kitaifa.

MATUKIO KATIKA PICHA





 

 Wimbo wa Taifa ukiimbwa wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.




Burudani zikiendelea wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.

Afisa Elimu mkoa wa Singida Mwalimu Nelas Mulungu akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.


 Afisa Michezo mkoa wa Singida Bw. Henry Kapella akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.


 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiteta jambo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari UMISSETA ngazi ya mkoa, mkoani Singida kwa kujumuisha wachezaji 700 kutoka halmashauri SABA za mkoa wa SINGIDA.

                                                         IMETOLEWA NA;
KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO 
OFISI YA MKUU WA MKOA
 SINGIDA.

No comments:

Post a Comment