Friday, December 02, 2016

RC SINGIDA AWAAGA VIJANA WAHADZABE 43 WANAOENDA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JESHI







Vijana 43 wa kihadzabe wakipunga mikono kuonyesha utayari wa kujiunga na kambi ya JKT Makutopora kikosi cha KJ 834 kwa hiyari kwa mkataba wa miaka ya miwili mara baada ya kuagwa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida. Jamii ya kihadzabe huendesha maisha yao kwa kuwinda na kula nyama pori, matunda ya porini, asali na mizizi.



Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida Bw. Buhacha Baltazar Kichinda ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya utawala na rasilimali watu akiwaaga Vijana 43 wanaojiunga na kambi ya JKT Makutopora kikosi cha KJ 834 kwa hiyari kwa mkataba wa miaka ya miwili. Bw. Kichinda amesema wakiwa jeshini watafundishwa uzalendo, ukakamavu, stadi za jamii na nidhamu, amewaasa wazazi kuwapeleka shule wanafunzi na kupokea fursa kama za jeshi.




Afisa Tawala ofisi ya Mshauri wa Mgambo Rhinocerus Magembesoni akiwaasa vijana 43 wa kihadzabe wakipanda mabasi kuelekea katika kambi ya JKT Makutopora kikosi cha KJ 834 kujiunga na kikosi hicho kwa hiyari kwa mkataba wa miaka ya miwili mara baada ya kuagwa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida. Jamii ya kihadzabe huendesha maisha yao kwa kuwinda na kula nyama pori, matunda ya porini, asali na mizizi.







Vijana 43 wa kihadzabe wakipanda mabasi kuelekea katika kambi ya JKT Makutopora kikosi cha KJ 834 kujiunga na kikosi hicho kwa hiyari kwa mkataba wa miaka ya miwili mara baada ya kuagwa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida. Jamii ya kihadzabe huendesha maisha yao kwa kuwinda na kula nyama pori, matunda ya porini, asali na mizizi.





Mmoja wa kijana wa kihadzabe Zuhura Ramadhani Longa ambaye alikuwa akiwasindikiza vijana wenzake wanawinda na kurina asali, amesema ameamua kujiunga na jeshi ili aweze kuisaidia familia yake lakini pia aweze kulitumikia taifa.

Vijana wa kihadzabe ambao walikuwa wanawinda na kurina asali, wamesema wameamua kujiunga na jeshi ili waweze kusaidia familia yake lakini pia waweze kulitumikia taifa.

No comments:

Post a Comment