Friday, April 26, 2024

RC DENDEGO AKONGA NYOYO ZA WANASINGIDA KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA...



Maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanafanyika hapa katika Wilaya ya Iramba na Kitaifa yanafanyika Dar es Salaam yakiwa na Kauli Mbiu Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania “Tumeshikamana na Tumeimarika, kwa Maendeleo ya Taifa letu”. 

Mkoa wa Singida unaungana na Watanzania wote katika maadhimisho haya kuanzia tarehe 14 April, 2024 hadi leo tarehe 26 April 2024 ambapo katika kipindi hicho shughuli mbalimbali zilifanyika katika Mkoa huo ikiwemo maombi na dua ya kuliombea Taifa, usafi katika maeneo ya Umma, michezo, Sanaa, utamaduni na kupanda miti kwenye maeneo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment