Friday, April 26, 2024

WANANCHI WA SINGIDA WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUWALETEA MAENDELEO MAKUBWA.

Wananchi wa mkoa wa Singida amesherekea miaka 60 ya Muungano kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuupatia mkoa wa Singida fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imeleta mabadiliko makubwa ya kijamii.

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego, akizungumza kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania ambayo kimkoa yamefanyika mjini Kiomboi wilayani Iramba amesema pamoja na Serikali Kuu kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo lakini bado kuna umuhimu mkubwa kwa wananchi kushirikiana na Serikali katika kujitolea nguvu kazi ili kuongeza kasi katika ukamilishaji wa miradi hiyo.

Dendego, amesema maendeleo ya kweli hayawezi kuja kama watu hawatashirikiana katika kufanya kazi hivyo ni muhimu kwa makundi yote kushirikiana kwa kiwango cha juu ili kuharakisha maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.

Aidha, amewahakikishia wananchi wa mkoa huo kuwa yeye ni muumini mzuri kwa watu wanaochapa kazi kwa bidii hivyo ni lazima wananchi wote kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.

Katika maadhimisho hayo ya miaka 60 ya Muungano, Mkuu huyo wa mkoa ametoa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika uandishi wa isha pamoja na vikundi mbalimbali vya burudani zilizotumbuiza hususan kwa wimbo maalum wa Muungano.

No comments:

Post a Comment