Halmashauri za Mkoa wa Singida zimetakiwa kutenga fedha
katika mipango na bajeti zake kwa ajili ya gharama za usafiri wa dharura kwa Mama
wajawazito na watoto wachanga.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter
Serukamba leo Novemba 22, 2022 wakati akifungua kikao cha Uzinduzi wa Mpango wa
Usafirishaji wa dharura kwa akina Mama wajawazito, waliojifungua na watoto
wachanga (M-Mama) kwa Mkoa wa Singida.
Rc Serukamba ameelekeza kwamba mfumo huo utakuwa ni msaada
mkubwa kwa wananchi wa Singida kwakuwa
utasaidia kupunguza vifo vya Mama
wajawazito, wanaojifungua na watoto kwa kuweza kufikishwa Hospitali au vituo
vya afya kwa wakati.
Amesema mpango wa huduma hiyo utaboresha zoezi la rufaa kati
ya vituo vya kutolea huduma za Afya, hasa upatikanaji wa usafiri wa dharura
kutoka kituo kimoja hadi kituo kinachoweza kutoa huduma ya viwango vya juu
ambapo ameeleza kwamba utasaidia kupunguza changamoto ya upungufu kusubiria
foleni ya magari ya wagonjwa.
“Kama tunavyofahamu huduma za Afya ya Mama na Mtoto hutolewa
bila malipo, kwa hiyo hatua mbalimbali za kuhakikisha huduma bora zinapatikana
katika Mkoa wetu wa Singida, ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vituo vya
kutolea huduma za Afya vinavyotoa huduma kamili za dharura na Upasuaji kutoka
vituo vya huduma sita (6) mwaka 2020 hadi saba (7) mwaka 2022” amesema
Serukamba
Kwa upande wake Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto Mkoa wa
Singida Christoweru Barnaba wakati akitoa wasilisho lake amesema mradi huo
utasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Aidha ameleeza kwamba
uwepo wa changamoto ya Upungufu mkubwa wa magari (Ambulance) za kubebea
wazazi na wagonjwa wanaohitaji rufaa hasa Halmashauri ya Itigi, Mkalama,
Singida, Ikungi kwa uwepo wa mradi huo utasaida kwa kuwa magari binafsi
yatasajiliwa kwa ajili ya kupeleka wagonjwa.
Akimalizia wasilisho lake Christoweru ametoa wito kwa mama wajawazito kuacha tabia ya kujifungulia
nyumbani au njiani na badala yake wahakikishe wanafika hospitalini ili waweze
kukutana na wataalamu.
Aidha Mkurungenzi wa
mfumo wa M-Mama Dolorosa Duncan kutoka Kampuni ya Vodafone foundation amesema Serikali kwa kushirikiana
na Vodacom inatekeleza mfumo wa rufaa na usafiri wa dharura – M-Mama ambao
umefanyiwa majaribio katika Wilaya za mkoa wa Mwanza na Shinyanga na kuona
unafanya kazi kwa ufasaha.
Hata hivyo Dolorosa ameendelea kueleza kwamba mfumo huo kwa sasa umeanza kutekelezwa katika mikoa ya Shinyanga Lindi Mororgoro Dodoma Tanga na sasa Singida na Manyara ambapo utaendelea kutekelezwa katika mikoa yote ya Tanzania bara na Visiwani.
No comments:
Post a Comment