Tuesday, April 26, 2022

Singida waadhimisha sikukuu ya Muungano kwa kufanya usafi

  

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Pasksi Muragili akiongoza zoezi la usafi wakati wa sherehe za Miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Wafanyabiashara wa vitunguu mkoani Singida leo wamepigwa marufuku kutumia  matumizi ya vifungashio ambavyo havijathibitishwa na Serikali na ambavyo vinazidi kilo mia kwa kuwa vinawapunja wakulima.

Akiongea na wafanyabiashara katika soko la vitunguu lililopo Kata ya Misuna mkoani hapo wakati wa zoezi la kufanya usafi Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Pasksi Muragili amewataka wafanyabiashara katika soko hilo kuachana  na matumizi ya vifungashio ambavyo havijathibitishwa na Serikali badala yake watumie vifungashio aina ya neti.

Amewataka viongozi wa Soko hilo kuwachukulia hatua wafanyabiashara wote wanaotumia vifungashio vyenye ujazo wa magunia unaozidi kilo Mia moja maarufu kama rumbesa kwa kuwa unawapunja wakulima.

"Serikali ilishatoka muongozo kuhusu matumizi sahihi ya vifungashio lakini nimepata taarifa kwamba bado wafanyabiashara wanaendelea kutumia viroba na magunia ambayo ni zaidi ya kilo Mia naomba kuanzia leo asiwepo mfanyabiashara anayetumia kifungashio zaidi ya neti ambayo imekubalika. Tunafanya hivi ili kuwasaidia wakulima wetu" Mhandisi Muragili.

Awali akihutubia wananchi walioshiriki shughuli za usafi katika soko hilo ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Muungano amesema zoezi hilo liwe endelevu na kila mtu awe na kawaida ya kufanya usafi katika maeneo yanayo wazunguka.

Mhandisi Muragili amebainisha kwamba Mkoa umejipanga kuhakikisha inaongoza kwa usafi hapa nchini na ndilo dhumuni la kuhakikishia usafi unafanyika kila siku.

Katika kuhakikisha zoezi linafikia lengo Mhandisi Muragili amemtaka Mkandarasi anayehusika na uzoaji la taka kuhakikisha wanaondoa vizimba vya taka kabla ya kufikia saa nae mchana wa leo.

Amesema anafahamu kwamba Mkandarasi anayesafisha eneo hilo la soko ana vitendea kazi vingi ikiwemo magari lakini hana vijiko kwa ajili ya kuzolea taka hivyo kumtaka akatafute ufumbuzi juu ya hilo ili aweze kusaidia kufikia lengo la kuweka Safi Mkoa.

Alimalizia hotuba yake DC Muragili akawataka wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la utoaji wa chanjo ya polio kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano tarehe 28 Aprili 2022.

Amewataka wananchi kushiriki zoezi hilo na kuwataka kuupuzia uvumi unaosemwa katika mitandao ya kijamii kwamba chanjo hiyo ina madhara, amesema wataalamu wa afia wamejiridhisha kwamba chanjo hizo ni salama kwa watumiao na inayoletwa kwa matone kwa watoto wote waliyopata au ambao hawajapata chanjo hiyo.

Amesema zoezi la chanjo hiyo limetokana na uwepo wa waathirika wa Polio katika nchiza jirani hivyo Serikali imeamua kuchukua tahadhari kwa kuwachanja watu wake ili kuepusha tatizo hilo. Alibainisha DC Muragili.

Alimalizia hotuba yake DC huyo amewataka wananchi wote kushiriki zoezi la Sensa ya watu na makazi itakayofanyika tarehe 23 Agost 2022.

Naye Mwenyekiti wa Soko la vitunguu Misuna Iddy Swalehe Mwanja akatumia nafasi hiyo kuiomba Wizara ya Kilimo pamoja na viwanda na Wizara ya viwanda na Biashara kusimamia zoezi la upatikanaji wa vifungashio vya kutosha uwezo wa kubeba kilo Mia moja kwa kuwa imeoneka kutopatika katika baadhi ya mikoa.

Amesema Singida wapo tayari kutumia vifungashio vya neti ambavyo havimpunji mkulima lakini ipo mikoa bado inaendelea kutumia rumbesa hivyo kusababisha wengine kukosa soko la vitunguu.

Swalehe ameendelea kuiomba Serikali kuyasimamia vizuizi vilivyopo barabarani kusimamia kikamilifu ukaguzi wa rumbesa ili kusaidia kuondoa changamoto za ujazaji wa bidhaa  wa kupitiliza.

Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali ya Serikalini pamoja na viongozi wa Soko na Wananchi mbalimba walikuja kufanya usafi wa maeneo hayo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment