Friday, September 21, 2018

Mkoa wa Singida leo umezindua Kampeni ya FURAHA YANGU



Mkoa wa Singida leo umezindua Kampeni ya FURAHA YANGU inayolenga kuhamasisha upimaji Virusi vya UKIMWI mkoani Singida.

Akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo kimkoa ambayo imefanyika katika Manispaa ya Singida, Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi amesema  Kampeni ya Furaha Yangu imejikita zaidi katika kutoa hamasa kwa wanaume na wananchi walio katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi ya VVU na kwenda kupata huduma ya ushauri na upimaji wa VVU na kuanza dawa mapema kama atakuwa amegundulika anaishi na maamukizi ya VVU.

Dkt. Nchimbi amesema, Kampeni hii itasaidia juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo ni kufikia malengo ya 90 tatu kama ilivyoelekezwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI, UNAIDS.

“Hii inamaanisha kwamba, mpaka kufikia mwaka 2020, asilimia 90 ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wafahamu kuwa wanaishi na VVU, asilimia 90 ya wanaoishi na Virusi vya UKIMWI watumie ARV kwa usahihi na uendelevu na asilimia 90 ya wanaotumia ARV waweze kufubaza Virusi Vya UKIMWI” Dkt. Nchimbi.

Amesema katika kufikia malengo haya, ni muhimu kwa Mkoa wetu wa Singida kila mtu akatimiza wajibu wake licha ya kwamba bado hali ya maambukizi katika mkoa wetu ni asilimia 3.4 ambayo ipo chini ya kiwango cha kitaifa (4.7%), kwa mujibu wa utafiti wa Viashiria vya UKIMWI hapa nchini vya mwaka 2012.

Aidha, amewaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri zote saba za mkoa wa Singida, kuhakikisha wanashirikiana na wadau mbalimbali kutenga maeneo ambayo wananchi watakwenda kupata ushauri na kasha kupima, na kama watagundulika kuwa na maambukizi waanze matibabu mapema kwa ajili ya kuwafanya wafurahie maisha.

“Naamini kwa kufanya hivi, Kampeni hii itafanikiwa na itachangia Dira yetu ya Singida bila UKIMWI inawezekana. FURAHA YANGU – PIMA, JITAMBUE, ISHI” Dkt. Nchimbi.

MATUKIO KATIKA PICHA












Kamishna Msaidizi idara ya Uhamiaji Mkoa wa Singida  Bi. Angela Shija akizungumza akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Daktari  Sisty Joseph Moshi kutoka Tanzania Health Support akizungumza kwa niaba ya wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Mganga Mkuu wa mkoa Singida Dkt. Victoria Ludovick akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Bw. Emmanuel Luhaula akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhandisi  Jackson Masaka akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.



Mheshimiwa Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akisalimiana na mwanamuziki Tunda Man aliyetumbuiza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.


Mkuu wa Wilaya ya Singida Bw. Pasacas Muragiri akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Huduma zikiendelea wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.


Mkuu wa Mkoa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (kulia) akimpongeza mwanamuziki maarufu nchini Tunda Man mara baada ya kutoa burudani wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.



  


Mkuu wa Mkoa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (watano kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki katika kufanikisha uzinduzi wa Kampeni ya FURAHA YANGU mkoani Singida.

Imetolewa na ;
Kitengo cha Habari na Mawasiliano
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
SINGIDA

No comments:

Post a Comment