Thursday, May 04, 2023

Kero lukuki Mnang'ana Ikungi zatatuliwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba leo ameendelea na zoezi la utatuzi  wa kero za  papo kwa hapo katika Wilaya ya Ikungi kata ya Sepuka Kijiji cha Mnang'ana  ambapo  kero 52 zilisikilizwa na kupatiwa ufumbuzi .

Akiwa Kijijini hapo RC Serukamba  alipokea kero za ukosefu wa maji, Barabara, migogoro ya ardhi na uharibifu wa maziringira ambapo alitoa maagizo kwa menaja wa RUWASA, TARURA na watendaji wa Serikali za vijijini na  kwenda kutatua kero hizo. 

Aidha RC amewaagiza wakandarasi wanaokarabati au kutengeneza Barabara kuhakikisha hawakati miti pasipokuwa na sababu kwa kuwa Mkoa upo katika utekelezaji wa kampeni ya kupanda miti na utunzaji wa mazingira ikiwa ni maelezo baada kuwasilishwa kwa kero ya ukataji miti ambayo haipo kwenye Barabara.

Hata hivyo Serukamba amewataka viongozi wa Serikali kwenye kata na vijiji wahakikishe wanawasikiliza wananchi na kutatua kero zao badala ya kukaa ofsini huku akiendelea kuonya tabia za watu unaowanyanyasa wanawake kwa kuwanyima haki ya kumiliki ardhi. 

Aidha, ameonya tabia za wafugaji kuchunga kwenye mashamba ya watu huku akizitaka kamati za vijiji kuangalia mabwawa ya kunyweshea maji na kuweka mkakati wa mifugo kutopita kwenye mashamba ya wakulima ikiwa ni pamoja na kulinda vyanzo vya maji kwa kupanda miti.

Zoezi la usikilizaji wa kero kwa mwezi Mei linaendelea kesho katika Wilaya ya Manyoni










Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba akikabidhi hati za kimili kwa wananchi wa Mnang'ana.

No comments:

Post a Comment