Wednesday, July 13, 2022

Serikali yadhamiria kuwaondoa wavamizi wa Msitu wa Mgori Wilayani Singida.

 

Mkuu wa Willaya ya Singida Mhandisi Pasikas Muragili akiongewa na wananchi wa kijiji  cha mughunga kuhusu marufuku ya serikali kuingia kwenye hifadhi ya msitu wa Mugori

Mkuu wa Mkoa wa Singida Binilith Mahenge akimiskiliza ,weyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida DC Eliya Digha walipotembelea Hifadhi ya msitu wa migori hivi karibuni kujione uharibifu unaoendelea.
wananchi wa Kijiji cha Mghunga wakimsikiza Mkuu wa Mkoa wakati wa ziara yake aliyoifanya  hivi karibuni alipokuwa akitolea ufafanuzi juu ya uvamizi wa mistu pamoja hatma ya wale waliondolewa katika eneo la hifadhi ya msitu.

Mkuu wa Mkoa akiendelea na Mkutano

Serikali imedhamiria kuwaondoa wavamizi wa Hifadhi ya msitu wa Mgori wenye ukubwa wa kilomita za mraba elifu 49 ambao umevamiwa na wnanchi kutoka maeneo mbalimbali kwa lengo la kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo ujenzi kilimo uvufugaji na uchomaji wa mkaa hivyo kusababisha  uharibifu mkubwa  wa mazingira.

Akiongea wakati wa ziara yake iliyofanyika hivi karibuni  katika hifadhi ya msitu huo Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge akiwataka wananchi wote waliovamia kuondoka wenyewe huku akiwataka wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) kwa kushirikiana na kamanda wa polisi Mkoa wa singida Kuhafanya doria na kuwakamata wote watakao kaidi agizo hilo.

RC Mahenge amesema, uharibifu wa msitu huo umeongezeka  ikilinganishwa na mwaka jana ambapo alijioea alipotembelea eneo hilo na kutoa maagizo ya kutolewa kwa elimu ili wavamizi waweze kuondoka wenyewe lakini bado hali imeendelea kuwa mbaya baada ya wengine kuja na kuanzisha makazi  eneo hilo.

“Si mara ya kwanza kutembelea msitu huu leo ni mara ya pili lakini naona uharibifu umeendelea kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na mwaka jana natoa maelekezo mengine kwa wakala wa huduma ya misitu Tanzania na TFS kwa kushirikiana na kamamnda wa polis mkoa kufanya doria katika eneo hili kila wiki mara moja na na nitafanya mawasiliano na wiazara ya maliasili na utalii ili kuona namna ambavyo wanaweza kuingiza msitu huu kwenye hifadhi zaio.” Alisema RC Mahenge.

 Aidha amemuelekeza Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Pasikas Muragili kuhakikisha ulinzi shirikishi unakuwepo kwa kuwashirikisha wananchi na viongozi wa vijiji vinazunguka msitu  ikiwa na pamoja na kuandaa mkakati wa muda mrefu wa namna ya kulinda msitu huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya  hiyo Mhandisi Pasikasi Muragili amemueleza mkuu wa mkoa huo kwamba walitoa elimu katika  vijiji vyote vinavyoizunguka hifadhi hiyo ikiwemo kuwachukulia hatua baadhi ya viongozi ambao walionekana kushiriki kuwaingiza waavamizia ndani ya msitu ambapo kesi zao bado zinaendelea.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Singida  Vijijini Elia Digha  akaiomba serikali kutilia mkazio ulizi wa msitu huo ambao kwa mkoa wa singida umebaki mmoja TU,huku akieleza kwamba tayari  wapo wananchi ambao wamevamia katika kijiji cha Muhunga kata ya Mgori wilaya ya singida.

Mwenyekiti huyo amesema kwamba zoezi la kuwandoa wavamizi hao limefanika Zaidi ya mara moja lakini inaonekana kuja wengine wapya jambo ambalo linahitaji ushirikiano baina ya serikali ili kulimaliza kabisa.

Hata havyo amesesisitiza kwamba wapo wananchi waliha ondolewa ambao bado wanasubuiria serikali kuwapatia eneo jingine la makazi na kilimo jambao ambalo Mwenyekiti huyo alibainisha kwamba serikali inaweza kulifikiria na kulitolewa majawabui ili wananchi hao waweze kufahamu kinachoendelea.

 

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya  Mughunga , Nassoro Hassan  amesema uvamizi wa msitu unasababishwa na ulizni mdogo ambapo doria ya mara kwa mara imeonekana kwuwa muoarobaini wa changamooto hiyo.

 Amesema wananchi wa kijiji chake wapo tayari endepo watapatiwa polisi hata  wawili kushiri kikamilifu kuwaondoa waavamizi hao kwa kuwa wamekuwa ni hatari hata kwa maisha yao kutokana na  wavamizi hao kutumia silaha za jadi kama upinde na mishale kupambana na watu wanaowazuia kuingia katika msitu huo.

Awali akitoa taarifa yake  kwa Mkuu wa Mkoa Muhifadhi wa Misitu wa Wilaya ya Singida, Uswege Mwasumbi  amesema tokea maagizo ya serikali ya kulinda msitu huo mwaka jana kutolewa wamchoma vibanda 704 vilivyokuwa vimejengwa kwenye hifadhi na kuwaondoa watu kwenye makazi hayo lakini inaonekana bado wanarudi au kuja wengine.

Amesema maelekezo yaliyotolewa na viongozi hao watayatekeleza ikiwemo ya kufanya doria ya mara kwa mara pamoja na kuchoma moto vibanda vitakavyojengwa na kuwafungulia mahstaka wote watakokuwa wamekamatwa katika msitu huo.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Mughunga  wameiomba serikali kuwapatia maeneo ya kulima na kujenga nyumba kwa kuwa wameondolewa katika eneo la hifadhi ambalo walingia kwa kutojua kama ni eneo la msitu jambo ambalo lilitolewa ufafanuzi na mkuu wa wailaya hiyo Mhandisi Pasikasi Muragili kwamba tayari wananendelea na utaratibu wa upimaji ili kuweza kuyatenganisha mazeneo ya makazi na  higfadhai

Hata hivyo RC Mahenge alitawataka waanchi hao waliokubali kuondoka katika eneo la msitu kuendelea na utulivu walionao wakati serikali ikiangalia  namna ya kuwapatia maeneo mengine mbadala.

Mwisho

 

 

No comments:

Post a Comment