Monday, May 20, 2024

WANANCHI ZAIDI YA 2687 WANUFAIKA NA HUDUMA ZA MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA, MKOANI SINGIDA

Wananchi zaidi ya 2687 wa mkoa wa Singida kutoka Halmashauri Saba za mkoa huo wamenufaika na upatikanaji huduma za matibabu ya kibingwa na bobezi kutoka kwa Madaktari bingwa 40 wa Rais Samia waliokuwepo katika mkoa wa Singida kwa muda wa siku Saba (7).

Kati ya idadi hiyo wananchi 69 wakiwemo watoto wamefanyiwa upasuaji kwenye Hospitali na Vituo vya Afya vya mkoa wa Singida badala ya kupewa rufaa kwenda kwenye hospitali kubwa.

Akipokea Taarifa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida kutoka kwa Madaktari bingwa kuhusu namna zoezi la utoaji wa matibabu lilivyofanyika, Katibu Tawala wa Mkoa Singida Dkt. Fatuma Mganga, amewapongeza na kuwashukuru madaktari hao kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa siku hizo kwa kuwapatia wananchi matibabu ya kibingwa na bobezi karibu na maeneo yao.

Amesema ujio wa madaktari bingwa na bobezi mkoani Singida pamoja na kutoa matibabu kwa wananchi wamesaidia kutoa elimu kwa Watalaamu wa afya wa kada mbalimbali hali ambayo itasaidia kuimarisha utoaji wa huduma za kiafya kwa wananchi wa mkoa wa Singida.

Kuhusu tatizo la upungufu wa Watalaam katika sekta ya afya, Katibu Tawala huyo wa mkoa amesema Serikali ya mkoa imejipanga vizuri ili kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi haraka ili wananchi waweze kupata huduma zote muhimu kwenye Hospitali na Vituo vya afya karibu na maeneo yao.

Nao baadhi ya Viongozi wa madaktari bingwa na bobezi waliokuwa wanatoa matibabu kwa wananchi mkoani humo wameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuanzisha mkakati maalum kwa Madaktari bingwa kwenda maeneo mbalimbali nchini ili kutoa matibabu kwa wananchi ambao hawana uwezo wa kusafiri kwenda kwenye hospitali kubwa kwa ajili ya kupata matibabu ya kiafya.

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA HAFLA YA KUWAAGA MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMI

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, akishangilia jambo wakati wa hafla ya kuwaaga Madaktari Bingwa wa Rais Samia iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida Mei 17, 2024.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Victorina Ludovick, akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga Madaktari bingwa wa Rais Samia iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida Mei 17, 2024.



Baadhi ya Madaktari bingwa wakitoa taarifa ya utendaji kazi wao wa utoaji huduma za matibabu ya kibingwa katika kipicho cha siku sita mkoani Singida kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, kwenye hafla ya kuwaaga Madaktari hao iliyofanyika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida Mei 17, 2024.





Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga (kushoto) akikabidhi zawadi na cheti cha pongezi kwa Madaktari bingwa wa Rais Samia, kwenye hafla ya kuwaaga Madaktari hao iliyofanyika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida Mei 17, 2024.








No comments:

Post a Comment