Monday, January 29, 2024

RC SERUKAMBA: WAKURUGENZI BIL. 5/-ZILIZOLETWA NA SERIKALI ZIPELEKENI HARAKA KWENYE MIRADI HUSIKA

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amewagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya mkoani hapa kuziondoa kwenye akaunti za halmashauri na kuzihamishia kwenye miradi husika zaidi ya Sh. bilioni 5 zilizotolewa na Serikali ili utekelezaji wa ujenzi wa miradi hiyo uanze haraka.

Ametoa agizo hilo leo  (Januari 29, 2024) katika kikao cha kufanya tathimini ya maendeleo  ya zoezi la uandikishaji watoto wanaojiunga na shule za awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza ambacho kiliwashirikisha Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Maafisa elimu kutoka halmashauri zote za mkoani Singida.

"Tumepewa siku 90 kukamilisha ujenzi wa miradi kutokana na fedha hizi tulizoletewa, kwa hiyo naomba fedha zote ziondoke kwenye halmashauri ziende kwenye miradi husika ili utekelezaji wa ujenzi uanze mara moja," alisema Serukamba.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza kuwa Wakurugenzi wote wanatakiwa kuonyesha fedha zote walizopata na kuainisha miradi gani wanakwenda kuitekeleza ili wananchi wa maeneo husika waweze kunufaika na matunda ya Serikali yao kwa kupata huduma stahiki katika maeneo yanayowazunguka.

Naye Katibu Tawala  Mkoa wa Singida Dk. Fatuma Mganga alisema Sh. milioni 350 zilizopelekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni zitumike kumalizia ujenzi wa bwalo katika Shule ya Wasichana ya Solya ili wanafunzi wa kidato cha tano na sita watakapoanza masomo wasipate tabu.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, akifuatilia jambo katika taarifa mbalimbali wakati wa kikao hicho.

Mkutano ukiendelea.




No comments:

Post a Comment