Wednesday, August 23, 2023

WATUMISHI SINGIDA WATAKIWA KUTUMIA MFUMO WA NeST KWENYE MANUNUZI YA UMMA

WATUMISHI wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Halmashauri za Wilaya na Manispaa mkoani Singida wametakiwa kutumia mfumo mpya wa ununuzi wa umma ujulikanao NeST ulioanzisha na Mamlaka ya Udhibiti na Ununuzi wa Umma (PPRA) ambapo mtumishi akifanya manunuzi bila kutumia mfumo huo atakuwa ametenda kosa la jinai.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Victorina Ludovick, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, alisema hayo kwenye mafunzo kwa watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoka halmashauri zote za mkoa huu kwa siku tano na kuwaeleza kuwa kutumia mfumo huo ni jambo la lazima kwani ni maelekezo mahsusi ya Serikali.

Ludovick alisema mfumo huu mpya wa manunuzi ni dhahili utaleta uwazi zaidi katika taratibu za manunuzi na utaongeza tija kwenye shughuli za Serikali hasa kwenye fedha ambako sehemu kubwa ipo kwenye manunuzi. 

Naye Mkuu wa Kitengo cha Menejimenti ya Ununuzi Sekretarieti ya Mkoa wa Singida, Nkuli Nketo alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo watumishi wa mamlaka za Serikali za Mitaa ili waweze kutumia mfumo huo mpya kuanzia Oktoba Mosi 2023 kwa lengo la kuepuka kufanya manunuzi ya aina yeyote nje ya mfumo wa NeST ambapo mfumo ulivyojengwa utawawezesha watumishi kufanya manunuzi ya aina yeyote ndani ya mfumo.

MATUKIO KATIKA PICHA

Mkuu wa Kitengo cha Menejimenti ya Ununuzi Sekretarieti ya Mkoa wa Singida, Nkuli Nketo, akitoa elimu ya matumizi ya mfumo mpya wa manunuzi (NeST) wakati wa mafunzo hayo kwa watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoka halmashauri zote za mkoa huo.


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA mkoa wa Singida, Baraka Mhembano akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo kwa watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoka halmashauri zote za mkoa huo.



Mkuu wa Kitengo cha Menejimenti ya Ununuzi Sekretarieti ya Mkoa wa Singida, Nkuli Nketo, akitoa elimu ya matumizi ya mfumo mpya wa manunuzi (NeST) wakati wa mafunzo hayo kwa watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoka halmashauri zote za mkoa huo.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria mkoa wa Singida Matrida Meckson, ambaye pia ni mmoja kati ya wakufunzi wa mafunzo hayo. 



Baadhi ya watumishi kutoka Mamlaka ya Serikali za mitaa wakiwa katika majaribio ya matumizi ya mfumo wakati wa mafunzo hayo. Kusho ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA mkoa wa Singida, Baraka Mhembano akifuatilia mafunzo hayo. 

No comments:

Post a Comment